Chombezo: Nipe kidogo sehemu ya tisa (09)
Maria alihudhunika sana kuona kashindwa kumuua mganga alichukia sana, akasubiri usiku ufike akutane na wenzake wapange mipango yakummaliza kabisa uyo mganga.
Siku iyo alishinda hana furaha kabisa mumewake alijua ilo akamuuliza anatatizo gani.
"Sina tatizo tena ukome kuniuliza maswali"
"Mmmh sawa"
Alijibu kiunyonge mzee kozi ambae alikuwa akifokewa kama mtoto anapokosea.
Maria alikuwa juu ya mumewake kwakila kitu mwanaume alikuwa kama zezeta afanyi lolote, chakula kikubwa kilichokuwa kikiliwa apo nyumbani kwao ni nyama ambayo haijulikani inatoka wapi!
Maria alipenda sana nyama ata ndugu zake wakija wanakula nyama adi wanatosheka.
Hatimae usiku ulifika kama kawaida Maria alinyanyuka nakuinama uvungu wa kitanda akatoa ungo wake nakujipaka unga mweupe usoni kisha akavua nguo zote nakubaki uchi akasogea adi kwenye pembe moja akaongea maneno kama kilugha ivi kisha akapotea nakutoka nje alipopanda ungo wake nakuanza kupaa juu.
Safari yake iliishia kwenye uwanja wa ruvu ambao ndio sehemu wanayokutana wachawi wote apo.
"Nina hasira sana kuna mtu nataka hauliwe leo hii na nyama yake iletwe apa tuile"
"Sawa usijali leo ni siku yakutaja matatizo yenu ilo linashughurikiwa sasa ivi andika jina lake dumbukiza mule kwenye mtungi"
Huyo ni kiongozi wao alisema.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Basi kila mtu mwenye shida yake akafanya ivyo ajabu akuna alietaka kuwa tajiri wala nini yani wote wanawaroga wengine kwa wivu wakimaendeleo
"Mimi nataka yule mangi duka lifirisike arudi kwao moshi"
"Mimi nataka mama juma mwanae asifaulu mwaka huu"
"Namimi shogayangu asiolewe yule bwana hamkimbie"
Matatizo ayo kila mtu aliandika lake wakaweka kwenye mtungi nakuufunika.
Yule mkubwa wao akaanza kuongea lugha za ajabu baada ya nusu saa alifungua mtungi nakuukuta mweupe hamna kitu kwani waliandika karatasi nakuweka humo ndani.
"Tusubirini majibu sasa"
Alisema wote wakakaa kungojea kuona uchawi walioutuma umeenda au imekuwaje.
Ghafla uchawi mmoja ulionekana kurudi kwa kasi sana waliogopa wote wakakimbia pembeni ule uchawi ukafika nakuupasua mtungi wao.
"Kunanini mkuu eeh imekuwaje?"
Waliuliza ata uyo mkuu alikuwa na hofu.
"Uchawi huu wa nani kwani?"
"Huu uchawi wakuua ni Maria mbona umerudi sasa kwanini?"
Walizidi kushangaa.
"Haiwezekani anishinde huyu twendeni kwake nikamuue kwa mikono yangu"
Alisema Maria wakaondoka wote adi nyumbani kwa mganga.
Walipofika walishangaa nyumba imezingirwa moto wakaanza kushangilia walijua nyumba inaungua lakini walipotizama vizuri ule moto wakichawi sio kawaida wakabaki kuguna
"Huyu uchawi wake wa n'gambo sio Tanzania"
"Wa wapi kongo au?"
"Ndio hatumuwezi huyu apo ukisogea tu umekufa"
Waliogopa wachawi wote wakaamua kuondoka ata kikaoni hawakurudi kila mtu akaenda nyumbani kwake.
Maria alizidi kupata hasira siku zote mchawi hakubali kushindwa
"Nitamkodia majambazi subiri adi afe huyu"
Alisema kwa hasira nakuingia ndani kulala.
*******************
Simu ya Brown ambayo alikuwa nayo monalisa iliingia mlio wa meseji ambapo alitoa simu ili hasome, ghafla simu ikapiga apo apo jina likaonyesha Sheby ikambidi monalisa ampe simu yake Brown aliepokea.
"Haloo nambie"
"Dah mshikaji kuna demu uku anakuulizia"
"Nani huyo? ebu ngoja tutaongea baadae"
Alisema Brown nakukata simu, akaingia inbox nakushangaa meseji imetoka kwa penny shemeji yake
"Brown naumia"
Akajiuliza anaumia nini hakupata jibu akaifuta nakuaga anaenda msalani alipofika uko akamwandikia meseji kumjibu.
"Penny niheshimu shemeji yako tena sahau kama umewahi kulala namimi nakaribia kuingia kwenye ndoa matatizo sitaki"
Alimaliza kuandika meseji nakutoka.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Jamani sisi ngoja tuwaache tuondoke"
Baada ya kukaa nusu saa akaaga Brown ambapo walisindikizwa adi nje nakuondoka zao.
Uku nyuma penny alikosa raha aliposoma ile meseji akaamua ampoteze Brown aliona ni ujinga mumewake akijua anaweza kumkata miguu sababu kilakitu alimpatia ata haki yake ya ndoa alipewa bila tatizo.
*****
Mipango ya ndoa ikaanza kupangwa mamayake monalisa alikuja Tanzania kushiriki vizuri harusi ya binti yake mpendwa.
Hatimae siku ya ndoa ilifika, kanisa la Mtakatifu Joseph lililokuwepo Posta watu wengi walijaa ndugu marafiki majirani padri Andrew Timthon ndie aliefungisha ndoa iyo. Baada yakumaliza maharusi walianza kutoka na watu wengine wakafatia sherehe kubwa iliandaliwa kwenye hotel yakifahari iliyokuwa ufukweni mwa bahari watu wote wakajaa apo walikunywa nakula adi usiku sana ulipofika bwana na bibi harusi walipoondoka kwenda kuanza honeymoon yao.
"Brown siamin umekuwa mumewangu"
Alisema Monalisa wakiwa chumbani
"Amini mkewangu nakupenda sana"
Brown alimsogelea nakumkumbatia mkewake mwisho wakaingia kuoga uku wakicheza kimahaba.
Walipomaliza walirudi kitandani kulala.
"Baby sogea uku"
Alianza uchokozi Brown kwa mkewake ambae alimkubalia wakabaki wanaangaliana kila mmoja akimtaman mwenzie.
"Mmmh lips zako laini ebu niziguse na mdomo wangu"
Brown alimwambia nakumsogelea kuanza kunyonya lips za mona aliesisimka sana zaidi ya nusu saa Brown alimchezea mkewe adi alipokuwa tayari ajabu sehemu zake hazikusimama alishangaa sana.
"Mona mkewangu angalia uku"
Ilibidi monalisa amtizame mumewe nakupigwa na mshangao kuona kumelala tu hakujainuka
"Unatatizo gani mumewangu jaman?"
Aliuliza ila hakupata jibu akainuka akaishika nakuweka mdomoni nakuanza kunyonya lakini haikusimama kabisa, ikabidi monalisa sasa amuandae mumewake zaidi ya nusu saa hali ilikuwa hiyo hiyo bila kutegemea Brown machozi yalimtoka kwa mara ya kwanza anajikuta akilia kwa uchungu sana tofauti ata ya kilio alichotoa siku aliyofiwa na wazazi wake.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hakuna kitu kinamuumiza mwanaume kama kukosa nguvu za kiume anaumia sana na iyo ndo ikamtokea Brown roho ilimuuma kushindwa kumpa haki yake mkewe.
Wiki nzima iliisha wakarudi nyumbani uku wote wakiwa hawana raha kabisa.
"Kwani tatizo nini mumewangu mbona nashindwa kuelewa?"
Aliuliza Monalisa
"Kiukweli atamimi nakosa raha kabisa sijui nini tatizo"
"Basi twende hospital ukachekiwe"
Alishauri mona,
Baada ya siku chache wakaenda kupima nakukuta Brown mzima kabisa hana tatizo lolote apo ndo alipogundua amerogwa sio bure.
"Naisi nimechezewa"
"Kuchezewa kivipi tena?"
"Ushirikina mkewangu"
"Mmmh mi siamini mambo ayo"
Monalisa alikataa kuamini.
Miezi ikazidi kusonga uku Brown akishindwa kumpa haki yake.
Mwezi wakujifungua ukafika monalisa akapata mtoto wa kiume alikuwa mzuri kama babayake!
"Asante mkewangu kunifanya niitwe baba"
Alisema Brown alipoenda hospital kumuona mkewe, baada ya siku mbili akaruhusiwa kurudi nyumbani maisha yakaendelea uku wakilea mtoto wao!
Miaka miwili akafikisha Beatrice ambae ni mtoto wao wakaandaa sherehe nakuarika ndugu na marafiki, mamayake monalisa pia alikuja walifurahi pamoja kwenye birthday ya Beatrice.
"Jaman namuomba mjukuu nikaishi nae mimi nyie tafuteni mwengine sasa"
Alisema kwa utani uku akicheka uyo mama hakujua mkwewake anamatatizo gani!
Basi alikubaliwa kizuri zaidi Beatrice hakuwa msumbufu nakunyonya aliacha.
Baada ya siku chache kupita wakiwa wenyewe tu Brown na Mkewe walianza kutafuta tiba za miti shamba!
Wakaenda ilala bungoni nakukutana na dokta mwaka walipata dawa nakuanza kutumia ila hali haikubadirika kabisa.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Wakajaribu kwa wataalamu wengine ilikuwa kazi bure adi mwaka unaisha Brown tatizo lake halikupona alikosa nguvu za kiume.
Akaanza kunywa pombe kilasiku analewa kazini hakwenda wala hakutaka kusikia ndani ya muda mfupi Brown alikonda nakuwa kituko.
Monalisa akawa mtu wakulia tu hakujua mumewake amepatwa na tatizo gani apo ndipo akaamua kumshirikisha kelvin ambae ni kakayake Brown alimuelezea yote bila kumficha.
"Inamaana tatizo limeanza siku ya honeymoon yenu?"
Aliuliza Kelvin
"Ndio shemeji adi sasa"
"Kwanini mlikaa kimya bila kusema?"
"Shem tulijua kawaida tu pia ni aibu jambo kama ilo kuongea"
"Sawa mtaalamu yupo na Brown atapona"
"Wow kweli Jaman?"
"Niamini shem wangu"
Basi walikubaliana wakapanga siku waelekee tanga handeni uko kwa mganga aitwae kiboko ambae ndo mtaalamu wake Kelvin kwenye biashara zake nyingi amemsaidia uyo mganga siku ikafika na safari ikaanza.
*******************
Maria alikumbuka kuhusu Brown yeye ndo aliempa mimba binti yake kisha akaikataa
"Brown hahahhhaa nimekukumbuka shenzi wewe ulikataa mimba ya jeni sasa nakufunga kizazi unajifanya rijali tuone nani atakutaka"
Ilikuwa usiku yupo mtupu chumbani kwake mumewake kampuliza dawa asiamke.
Akachukua kioo nakuongea maneno mengi sura ya Brown ikatokea apo
"Hahahhhaa Brown ukose nguvu za kiume kuanzia sasaa"
Alisema kwa sauti kubwa akicheka sana.
Basi alipomaliza akavaa nguo nakutoka kwenye hali ya uchawi akaingia kitandani kulala.
Kulipokucha aliwahi kuamka nakufanya kazi zake zote nyumbani uku mumewake akienda vibaruani.
"Hee nimemkumbuka mwanangu priska jaman"
Alisema Maria uku machozi yakimtoka
Kumbe anamtoto mwengine lakini hakuzaa na huyu mumewake.
Akazidi kukumbuka kipindi iko kabla ajawa mchawi aliolewa na mumewe akawa mkorofi akimpiga sana mwisho akakimbia nakumuacha mtoto wake wa miaka mitano ambae ndo huyo priska.
"Lazima nimkomeshe yule shetani nyama yake nitafune yote alinitesa sana"
Alisema kwa hasira sana akakumbuka siku anayokabidhiwa uchawi na babayake mzee Marcus
"Baba mi siwezi sitaki kuwa mchawi"
"Hahahhahaaa wewe ndio mrithi wangu lazima ukubali na ukikataa nakutoa kafara"
Alisema nakumtisha ikambidi akubali tu.
mwanzo alikuwa muoga ila kadri siku zinavyosonga akazoea nakuwa gwiji wa wachawi adi cheo akapewa kabisa.
BONYEZA HAPA UPATE MESEJI NZURI ZA MAPENZI
INAENDELEA

No comments