Header Ads

Header ADS

Simulizi: Safari sehemu ya kwanza (01)

 




Mwandishi E. MBOGO

#1. Kilikuwa kipindi cha ukoloni karne ya 15 katika ngome kongwe ya mfalme MWAMAKUNGE ilikuwa ni ngome iliyoogopeka kwa uendeshaji wa mfalme huyo kwani alikuwa katili kupita kiasi aliuwa watu na kuteka wakoloni kutoka ngome nyingine basi alijulikana mno na kuogopeka kipindi hicho kwani alikuwa na vijana wachapakazi na waliobobea kwenye mapambano na waioiva kisawasawa. Wafalme wenzake walikuwa wakija kununua watumwa kutoka kwake basi alitokea mfalme alie taka watumwa kazaa wenda kusaidia katika kijiji chake kwani kulikosa msaada basi ilimbidi aje kuomba msaaha kwa mfalme MWAMAKUNGE katiriiiii lao basi ilimpasa mfalme MGAZA kuja kuomba iliii aweze kumpa msahada wa watumwa wachache.

Ilikuwa asubui na mapema ndipo vijakazi wa mfame MWAMAKUNGE walipoona jahazi kwa mbali zikija kwenye eneo lao basi walipiga kengeree kuashiria kuwa makini kwa kila mtu aliyepo maeneo hayo au kwenye ngome hiyo basi vijana walijificha na kutazama msafara huo mpaka ulipofika.

Ulipofika mfalme MGAZA alishuka huku akiwa na mlinzi wake na ndipo alipoo omba akutanishwe na mfalme MWAMAKUNGE nae alijitambulisha na vijana walichomoka na kufikisha habari kwa mfalme wao na ndipo alipofika nae alipooo mwona mfalme MGAZA alimfahamu mara moja na aliruhusu vijana kuingia ndani ya ngome.

Basi alipofika kwa mfalme MWAMAKUNGE aliongea nae kuhusu msahada aliokuwa akiitaji kutoka kwenye falme yake.

MWAMAKUGE" karibu sana hapa nyumbani vipi kurikoni mbona asubui mnooo lete habari za hapa na pale huko utokako"

MGAZA "mmmmmh huku nitokako hali si shwari kwani naitaji msahada wako kwa garama zote utakazo"

MWAMAKUNGE "kitu gani hicho nijuze nami nitakusaidia wala usiwe na shaka"

MGAZA "haaah shida yangu ni kuniongezea watumwa wapatao 500 japo nikaongeze hata nguvu ya utenda kazi kwani vitu huko vimesimama kukosa watenda kazi"

MWAMAKUNGE "hooooh sawa lakini siunajua kuwa huwa natoa kwa pesa basi nikatie mafungu yangu nihamlishe wakuleteee huondoke mapema"

Walikubaliana na ndipo mfalme MWAMAKUNGE alipo wahamuru vijakazi wake wawa danganye watumwa kuwa wanarudishwa kwao.

Basi walifanya kama alivyooo sema mfalme MWAMAKUNGE huku wafalme hao wakigawana walicho kubaliana pembezoni kidogo huku wakielekezana


 Ni njisi gani watawaingia kiurahisi, na kuamini wanarudishwa kwao bali

walikuwa wakiuzwa nakupelekwa sehemu nyingine, yote hayo hawakujua kwani kila

mtumwa alitoa tabasamu zuri, huku akiwaza kuonana na ndugu zake toka walipo

hachana muda mrefu, pindi walipo tekwa na ufalme wa MWAMAKUNGE katili lao.

Mfalme MGAZA alimpatia pesa zenye dhamani ya watumwa aliopewa, na huku kwa

urafiki wao mfalme MWAMAKUNGE alimpa watumwa wengine kidogo, kuonesha urafiki

wao huku akimwonesha kwenye majahazi waliokuwa wakipanda watumwa hao.

Basi mfalme MWAMAKUNGE ndipo alipo muaga mfalme mwenzake, kwa safari yake ya

kurudi kwenye ngome yake, na ndipo mfalme MGAZA ali amuru vijakazi wake waanze

safari mara moja, na safari ilianza kwa kasi msana, huku watumwa wakitizama

ngome ya mfalme MWAMAKUNGE, kuiacha na kufurahi sana, huku wengine wakishusha

pumzi nzito kwa uchovu wa kazi walizokuwa wakifanya, na mateso makubwa ya siku

zote, awakujua waendako, pia hawakujuwa kama kule wanako kwenda, ni kazi kama

walikotoka, hayo yote hawa kujua, laiti wangelijua waendako ndiko kuna mateso

zaidi, wangeli panga njia ya kutoroka pindi safari hiyo ilipokuwa ikishika

kasi baharini.

INAENDELEA

No comments

Powered by Blogger.