Simulizi: Rama sehemu ya tano (05)
Niko sawa, niko kwaajili yako, nimeamua wewe ndiyo mwanamke wa maisha yangu.” Nilimuambia huku nikimsogelea na kumkumbatia, alinishika na kunitomasa, alinichezea kila sehemu ya mwili wangu lakini nilikua wa baridi kama vile nimemwagiwa kwenye friji, akili zangu hazikua pale, nilikua namuwaza mke wangu mpaka uume wangu ulishindwa kusimama kabisa.
“Au una muwaza mke wako?” Aliniuliza, ingawa ilikua ni kweli lakini niliona aibu kukubalia, nilitingisha kichwa kumkatalia.
“Nadhani ni kwakua ni mara ya kwanza hatujazoeana, nina ihakika mpaka subuhi tutaweza.
Nilimsogeza karibu yangu na kumkumbatia, nilichukua simu yangu na kuanza kupiga picha.
“Unafanya nini?” Aliniuliza, nilinyamaza sikumuambia chochote, niliendelea kupiga mpaka aliponinyang’anya simu, tulikua uchi kitandani na nilikua nataka kupiga naye picha.
“Unafanya nini wewe? si unajua kuwa unha mke, akija kuziona?” aliniuliza, nilimkumbatia vizuri kwa nguvu, nilijikuta nasisimkwa, hata yeye alishangaa, alicha wazo la picha na kuanza kunikumbatia, simu ilikaa pembeni tukaanza kufanya yetu. Kwa mara ya kwanza nilimsaliti mke wangu na nilijisikia vizuri sana.
Weekend ile ilienda vizuri sana, tulifurahia na tulifanya kila kitu, nilirudi nyumbani nikiwa nimechangamka. Lakini niliporudi sikumkuta mke wangu, naye alikua katoka, nilipomuuliza Binti wa kazi alinijibu kuwa alitoka siku ile tu nilipoondoka na alikua hajarudi. Kumbuka weekend nzima sikumpigia simu mke wangu, nilifanya hivyo ili kumuumiza, lakini naye hakunitafuta, kumbe naye aliondoka, nilichukua simu na kuanza kumpigia, nilipiga mara ya kwanza simu haikupokelewa, nilipopiga mara ya pili ilipokelewa lakini hakua mke wangu, ilipokelewa na Mama mkwe wangu.
Moyo ulitulia kidogo, mwanzo nilihisi kama mke wangu kaenda kwa mwanaume mwingine tena na mtoto, alipopokea Mama yake nilimsalimia na kumuulizia mke wangu. Aliniambia kuwa yuko salama lakini hawezi kuongea na mimi kwani namfanyia vituko na kashajua kuwa nina mwanamke mwingine hivyo anahitaji nimpe talaka.
“Yessssss!” Nilijikuta napiga kelele kufurahia.
“Unasemaje?” Mama mkwe aliniuliza, nilinyamaza kwani kelele zangu hazikua sababu ya mke wangu kudai talaka bali nilifurahi kuwa hatimaye nimefanikiwa kumuumiza mpaka akaenda kwa Mama yake.
“Mimi Mama talaka siwezi kutoa, mke wangu bado nampenda, najua kuoa lakini sijui kucha!” Nilimuambia huku nikikata simu, nilijua kabisa kuwa nimewaumiza, nilijua kuwa mke wangu kakasirika na kajua kuwa mimi nachepuka ndiyo maana kaenda kunishitaki kwa Mama yake. Nilikata simu nikijua kuwa watanipigia ili kunibembeleza, lakini haikutokea hivyo, nilisubiri na kupiga tena usiku, alipokea Mama mkwe wangu na kuniambia kuwa mke wangu hawezi kupokea simu zangu kwani ameumia sana anachosubiri ni talaka yake basi.
Nilifurahi sana, sikua na mpango wa kumaucha mke wangu lakini nilijua namimi nimeweza kumuumiza. Nilimuambia Mama mke kua siwezi kutoa talaka, nilikaa kimya kwa siku tatu bila kuwatafuta lakini nao hawakunitafuta, nilianza kuwa na wasiwasi nikidhani kuwa labda mke wangu kweli alikua akimaanisha, niliamua kumpigia tena simu mke wangu ili kumuomba msamaha na kuacha yaishe. Nilipiga simu ikaita sana lakini haikupolekewa, iliita sana mpaka kukatika lakini kila ilipoita nilizidi kupiga, nilijihisi kuchanganyikiwa kwani niliona kama mke wangu ananiacha.
Mwisho mke wangu alipokea simu, alikua akilia sana huku akinilaumu mimi kuwa yeye kaamua kubadilika lakini mimi simuoni nimeamua kuwa Malaya.
“Najua unalipa kisasi lakini magonjwa ni mengi, nimechoka wewe kunirudia usiku wa manane, nataka talaka yangu sitaki tena kuishi na wewe!” Mke wangu alilalamika, nilimbembeleza sana lakini hakutaka kunisikia, alikua akidai talaka na kusema kuwa hawezi kurudi tena kwangu. Tulishindwa kuelewana na kuamua kumpigia simu Mama yake, nilimuambia nikweli nilikua na mtu lakini ni rafiki tu na nilifanya hivyo baada ya mke wangu kunisaliti. Mama mkwe naye alikua upande wa mwanae akidai nimpe talaka.
Nilikataa katakata, siku hiyo hiyo nilipanda gari kuelekea tanga, nilifika usiku hivyo sikufika moja kwa moja kwa Mama mkwe wangu. nilienda kwenye nyumba moja ya kulala wageni, lakini usiku huo huo nilimtafuta mzee mmoja ambaye alikua ni kama mshenga kwangu, yeye ndiyo ambaye mara nyingi alikua akinipokea nikienda tanga kwani kipindi Baba yangu ni Askari Tanga alikua ni rafiki yake mkubwa. Kwanza alishangaa kuniona, nilimsalimia na kumuambia swala langu, kumuambia nilipokua nimekosea na kumuomba kesho yake kuongozana mpaka kwa mke wangu ili kuomba msamaha.
“Msamaha wa nini tena, kama ulitoa talaka hakuna cha msamaha tena…” Aliniambia.
“Hapana Baba, mke wangu bado sijampa talaka, ameondoka tu bila kuniaga.” Nilimjibu, aliniangalia kwa mshangao zaidi, aliniuliza mara mbilimbili kama nilimpa talaka au la lakini nilikataa.
“Mbona sielewi sasa, maana leo tu ndiyo nimetoka kule, kuna watu walikuja kutoa mahari nikajua labda mshaachana! Hii familia vipi ndoa juu ya ndoa, hata mume wake wa kwanza sidhani kama alitoa talaka, yule mwanaume alifukuzwa tu kama mbwa baada ya wewe mwenye pesa kuja!”
“Mume wake wa kwanza?” Nilimuuliza, yule Baba aliniangalia kwa mshangao.
“Inamaan hujui kuwa mke wako alishawahi kuolewaga na ana mtoto mkubwa tu?” Aliniuliza swali ambalo liliniacha mdomo wazi.
***
Ninakua na wateja wengi hivyo kumjibu kila mtu anayenitumia SMS ni ngumu, kama unahitaji ushauri ni lazima uwe umenunua vitavu vyangu, kama unahitaji ushauri wa mahusiano ya kawaida nilazima uwe umenunua Kitabu cha “Ndoa yangu Furaha Yangu” Bei yake ni Shilingi elfu kumi tu!
Kama ushauri unahusiana na mapenzi lakini unagusa upungufu wa nguvu za kiume wa mwenza wako au wewe mwenyewe mwanaume au maumbile madogo na namna ya kumrishisha mwanamke basi Kitabu ni “MWANAUME” bei yake ni Shilingi elfu ishirini.
RAMA; MAMA YENU AKIRUDI NAOMBA MUMUAMBIE KUWA MIMI NIMETOKA!---SEHEMU YA SITA
Suala la mke wangu kuwa na mtoto nilishalihisi, alikua akifanana sana na yule mtoto na mara zote alikua akimuita Mama. Mke wangu alikua akiniambia nikwakua yeye ndiyo kamlea lakini namna alivyokua akimjali ilikua ni zaidi ya mtoto wa ndugu yake. Lakini suala la kuolewa kabla lilinichanganya zaidi, sikutaka kuamini lakini namna yule mzee alivyokua akiongea na matukio ya mke wangu nilijikuta naamini. Niliumia sana kwani nilikua nampenda sana mke wangu, alishanifanyia mengi lakini nilimsamehe kwasababu ya upendo wangu kwake.
“Ukitaka amani mpe tu talaka, andika tatu aendelee na maisha yake…” Yule mzee aliniambia, aliongea kana kwamba kilikua ni kitu kidogo sana, mimi tayari nilishanganganyikiwa, hata kukaa pale niliona shida, niliondoka kama mtu aliyechanganyikiwa na kwenda mpaka nyumbani Kwa kina mke wangu. kila mtu alishangaa kuniona lakini cha ajabu walinikasirisha vizuri tu, katoto ka mke wangu kalikuja kunisalimia Baba, mke wangu aliniangalia kwa aibu, Mama yake alikua kimya na ndugu zake wengine walikuja kunisalimia.
Ukimya ulitawala, kila mmoja alikua akimtegea mwenzake ili kuongea, baada ya kuona ukimya umezidi niliamua kuuvunja.
“Nimekuja kukuchukua, wewe ni mke wangu mimi siwezi kukupa talaka! Kwa kosa gani hasa mpaka mimi nikuache!” Nilianzisha mazungumzo.
“Umemsaliti mwanangu, wewe si una mwanamke wako, sasa kwanini hutaki kumuacha mwanangu!” Mama mkwe aliongea kwa hasira, mke wangu bado alikua kanyamaza, alikua anajua kuwa sijamkosea chochote, mambo yote niliyokua nayafanya yalitokana na tabia zake.
“Hapana Mama, mwanao kanifanyia mambo mengi mabaya, lakini nimesamehe, mimi kosa moja tu ndiyo anajifanya kuniacha, siwezi kumuacha mke wangu nampenda sana!” Niliwaambia, yalizuka mabishano makubwa kati ya mimi na Mama mkwe wangu, yeye alitaka mimi na mke wangu tuachane. Wakati wote huo mke wangu alikua kimya, alikua akiangalia chini, akijifanya kuwa ana aibu na kujifanya kuumizwa na yele mambo, nilijua janja yake, alitaka kuonekana kama mwema na mimi kuona kama ndiyo mwenye tatizo.
Sikutaka kuuliza kuhusu habari za yeye kuolewa tena, si kwamba kile kitu kilikua hakinikerteketi lakini nilikua sijamuamini sana yule mzee, lakini nilitaka mke wangu kuniambia yeye mwenyewe. Nilimdodosa sana ili kuniambia sababu za kutaka kuachana na mimi lakini hakutaka, hata Mama yake hakusema, walizidi kusingizia tabia zangu huku mke wangu akisema kanichoka anataka nimpe talaka.
“Una hangaika nini? Kwani talaka basi ni lazima akupe, akikutamkia tu ni kama kakuacha!” Mdogo wake wakiume aliongea, nilimuangalia kwa hasira na kumuambia.
“Mimi dada yako sijamuacha, kama ndiyo mipango yenu basi mmechina, sijamuacha mke wangu si kwa maneno wala si kwa maandishi, huyu ni mke wangu na nimakuja hapa kwa njambo moja tu ambalo ni kumchukua.”
“Nilikuambia tu kiheshima ili uniache lakini mimi nilishaachika kwako muda mrefu. Mimi sisalitiwi na kwa taarifa yako talaka ulishanipa tena tatu…” hatimaye mke wangu aliongea, wakati nabishana na ndugu zake alitoa kipande cha karatasi, kilikua na muandoka wangu na saini yangu kuonyesha kuwa mimi nimemuacha mke wangu tena kwa talaka tatu.
Kama alivyofoji sahihi yangu katika kuuza gari ndivyoa livyofanya kwenye talaka.
“Kwahiyo nikweli unataka kuachana na mimi?” Nilimuuliza, baada ya kuona kile kikaratasi ndipo niliamini kuwa mke wangu anataka kunicha. Nilikua naumia sana lakini kama alishafikia hatua ile nilijua ndiyo basi.
“Ndiyo, nimeamua nimechoka na tabia za….” Alijaribi kujitetea hukua kijifanya kulia lakini sikukubali anisingizie.
“Hapana, wewe unajua kila kitu, utadanganya kila mtu kuniumiza mimi lakini kumbuka kuwa mimi na wewe tunaujua ukweli, machozi yako hayasaidii, umeniumiza sana na kama kweli umeamua basi baki na mimi naendelea na maisha yangu.”
Niliongea huku nikinyanyuka kwa hasira, niliona aibu, nilijisikia vibaya, pamoja na kumpenda sana mke wangu lakini niliona kuwa ameshaamua, sikua na haja tena ya kumtetemekea, kumlilia wakati hanitaki. Niliingia kwenye gari nikaenda sheli na kujaza mafuta kisha nikarudi zangu dar siku ileile. Sikutaka tena kusubiri, akili ilikua haiku sawa. Nilifika bila kupumzika nilimtafuta Joan, nilimuomba kuja nyumbani, alishangaa ni kwanini lakini nilimuambia kuwa mke wangu nimemfukuza.
“Nimechoka tabia zake, nimemuacha na sasa nataka kuanza upya.
Niliumia sana lakini kama mwanaume nisingeweza kusema kuwa nimeachwa, nilijifanya kumuacha mke wangu, kila rafiki yangu, kila ndugu nilimuambia kuwa nimempa mke wangu talaka tatu. Katika kipindi hicho ndipo niligundua madudu mengi ya mke wangu, kila mtu sasa alianza kufunguka.
“Afadhali umemuacha, alikua anatembea na flani….mimi nilishamuona sehemu flani akiwa hivi na vile…nina wasiwasi hata yule mtoto si wako…nilishawahi kumfumania,….yule si mwanamke” Nilisikia madudu mengi sana ya mke wangyu, alitembea na zaidi ya nusu ya marafiki zangu, alishatembea mpaka na Baba yangu mdogo na vite nilisikia baada ya kusema kuwa nimemuacha.
Ingawa kila mtu alikua ananipongeza lakini sikua na amani, hongera zao zilikua kama dhihaka kwangu, nilijisikia vibaya walivyokua wakiniambia kuwa ni Malaya, niliumia kwakua bado nilikua nampenda, nililia, nilihuzunika lakini nilificha huzuni zangu. Sikutaka watu wajue na kwakua nilikua na joan wangu nilimfanya kama mke, nilikua nikifanya naye mapenzi kila siku, kwangu ilikua kama kazi, kilikua ni kitu cha kunifanya nimsahau mke wangu kwa muda flani, sikua na furaha pamoja na Joan kufanya kila kitu ili kunifurahisha.
Bado nilikua na hasira na mke wangu, nilitaka kulipa kisasi, nilitaka kama mimi nilivyoumia yeye naye aumie. Lakini nilimuona kama vile haumii, alikua kawaida kabisa anaendelea na maisha yake, alikua hanitafuti na kila siku alikua akipost picha facebook kuonyesha kuwa ana furaha. Niliumia hivyo na mimi nilitaka kumuonyesha kuwa nina furaha, nilianza kumtumia picha zangu nikiwa na Joan, kipindi hicho ilikua ni Facebook tu ndiyo ina nguvu, sikutaka kumpost Joan kwani sikutaka watu wengi kujua kuwa niko naye.
Lakini nilitaka mke wangu ajue hivyo nilimtumia picha zangu na joani kila safari, kila starehe, picha za kitandani, picha tukifanya mapenzi na kila kitu lengo lilikua kumuumiza lakini niliona kabisa kuwa haumii. Hakuniblock zaidi ya kunidhihaki kwa kumsifia Joan kinafiki, hali hiyo iliniumiza sana, nilikosa amani ingawa mimi ndiyo nilikua namtafuta na kumsumbua lakini nilimblock ila baada ya muda nilifungua akaunti nyingine feki na kuanza kumfuatilia tena. Hali ilikua mbaya sana kwangu mpaka joani akagundua kuwa namtumia yeye ili kumsahau mke wangu.
Alijua kabisa kuwa si mimi niliyemuacha mke wangu bali ni mimi nilikua nimeachwa, alikasirika na kuondoka, hakutaka kuja kwangu tena, alidhani nitamuomba msamaha lakini wapi, sikua tayari kwa hilo. Baada ya Joan kuondoka na kuwa kama vile kaniacha kisirani kilizidi, hasira zilizidi na nilitaka kulipa kisasi. Nilifikiria njia nyingi za kulipa kisasi nikajua ili mke wangu nayeye asiwe na amani nimharibie kwa mchumba wake mpya, ingawa alifanya siri nisimjue lakini nilihangaika mpaka nikampata, yeye alikua dar, alikua na kampuni ya maji na pia alikua na hoteli mbili kubwa tu.
BONYEZA HAPA UPATE VICHEKESHO BUREE
INAENDELEA

No comments