Simulizi: Rama sehemu ya tisa (09)
“Sitaki kusikia, wakati anatembea na wewe alijua kabisa kuwa wewe ni mume wa mtu lakinia kajilegeza mpaka kupata mimba, hiyo mimba ni yake si yako, haituhusu na kama ni mtoto basi si lazima kumpigia simu, unaweza kutuma pesa kwenye M-Pesa na mtoto akalelewa huna hjaja ya kumuona Mama yake au kuongea naye. Ni uchague kayi yangu na huyo mwanamke, mimi siwezi kuchanganywa kama hunipendi uniambie kabisa nijiondokee zangu.” Aliongea kwa hasira, nilimkubalia kuwa nitaacha kuongea na Joan na nitakua nikutuma pesa bila hata kumpigia simu.
Niijua yameiha alitoa simu yake alipiga namba ya simu na kunipa simu.
“Nini? Nani huyo?” Nilimuuliza.
“Huyo mwanamke wako, nataka uongee naye muambie kabisa kuwa humtaki, asikutafute tena uko na mke wako na kama ni matumizi nitakua nikituma mimi na si yeye.” Sijui alipata wapi namba yake lakinia likua tayari ahsampigia Joan, nilisikia Halloo ya upande mwingine. Nilikua sijapanga cha kuongea, nilitaka kukata simu lakinia aliniambia kabisa nichague kati ya yeye na Joan, kama nikikata ndiyo basi mapenzi mimi nayeye. Nilikua nampenda sana mke wangu, nilishindwa kukata simu,niliichukua na kumuambia Joan kila kitu nilichokubaliana na mke wangu, nikaongea naye mbele ya mke wangu kisha niakakata simu.
Joan alinipigia katika simu yangu, mke wangu aliipokea na kuanza kumtukana, alimtukana sana matusi ya nguoni mpaka nikawa nakasirika lakini sina chakufanya. Joan aye alikua akitukana hivyo walianza kutukaana mpaka nikaona aibu nikaondoka nikatoka kwenda kulala sebuleni. Sikurudi ndani mpaka asubuhi yake ambapo mke wangu alitoka kwa hasira, alianza kulalamika kuwa Joan kamtukana sana na ni kosa langu hivyo natakiwa kuchagua kati yake na Joan, nilimuambia nimemchagua yeye ndipo aliniambia kuwa kwa namna alivyotukanwa siku akiniona na wasiliana na Joan basi ndiyo mwisho wa ndoa yetu kwani nitakua nimemdhalilisha sana.
Nililazimika kukubaliana na mke wangu kwani hata nilipomtafuta Joan hakutaka kuongea na mimi, sliishia kuniambia kuwa wewe tunza mwanao sitaki mawasiliano nawe huyo mwanamke wako ni mshenzi sitaki kujihusisha naye. Baada ya hapo hakutaka mawasiliano na mimi, lakini hata mimi nilijitenga naye, sikutaka kumuudhi mke wangu, mwanzo nilikua nikituma pesa nampigia simu kumuuliza kama amezipata au la ila baada ya muda niliacha kumuuliza. Nilimblock kila sehemu na kuwa natuma pesa kwa wakala tu, wakala akinithibitrishia kuwa zimefika basi naridhika maisha yaliendelea.
Mwaka mzima ulipita bila kuwasiliana na Joan, nilianza kuona kama kitu cha kawaida, ndugu zangu walipokua wakiniuliza kuhusiana na mwanangu niliishia kuwaambia kua anaendelea vizuri ingawa nilikua sijui chochote kuhusu yeye. Maisha yalikua ya amani kidogo kitu pekee ambacho kilinitesa ni mke wangu kukataa katakata kuachana na yule Baba akisema hawafanyi kitu kibaya chochote. Niliumia lakini angalau alikua hachepuko na watu wengine, baada ya kuwa na yule Baba mke wangu alikua na heshima debe, alikua si mtu wa kunywa pombe sana kama zamani ingawa bado hakutaka kabisa niende dukani akisema ni sehemu yake ya kazi mbona yeye haji kwangu.
Mwanangu alipofika Darasa la pili mke wangu alilazimishia kumpeleka Bweni, alisema shule aliyokua anasoma si nzuri na anataka kumhamisha. Ingawa sikupenda lakini alilazimishia sana ili kukwepa kelele niliamua kukubali. Alifuatilia uhamishio wa kila kitu na kumpeleka shule nyingine, kila kitu alifanya mwenyewe mimi alinipa tu taarifa. Aliniambia tu kwamba mtoto kampeleka shule flani lakini hakuniambia chochote kingine. Wiki mbili tu baada ya kumpeleka mtoto wetu shule nilienda shuleni kwao, sikupanga lakini kuna mfanyakazi mwenzangu ambaye naye mtoto wake alikua akisoma katika ile shule, alianguka darasani ghafla hivyo alipigiwa simu na mimi ndiyo nilimpeleka.
Kwangu niliona kama fursa ya kumtembelea mwanangu, nilifika na kweli nilimuona mwanangu, aliponiona tu alinikimbilia kunisalimia. Mtoto aliyedondoka alikua anaendelea vizuri lakini Baba yake aliombva kumchukua ili kwenda kumpeleka hospitali kubwa kuchekiwa vizuri. Wakati tunaondoka mtoto wangu alining’ang’ania na kutaka tuondoke wote, niliwafuata walimu kumuombea na kutaka kwenda naye ntamrudisha jioni.
“Hapana huruhusiwi kumchukua, hata kama ni ndugu lakini mtu aliyeandikwa hapa ndiyo anaruhusiwa, Baba yake au Mama yake.” Mwalimu aliniambia, kwakua nilikua sijawhai kufika pale niliwaelewesha kuwa mimi ndiyo Baba yake.
Aliniomba kitambulisho changu ili kuangalia jina, nilikitoa bila wasiwasi wowote.
“Hapana, mbona jina la Baba na hata picha sio wewe. Anahtajika Baba mzazi si Baba mdogo au Baba mkubwa.” Mwalimu aliniambia, niliwaka kidogo mpaka akanionyesha kwenye Mfumo wao jina la Mama lilikua la mke wangu pamoja na Picha yake. Lakini jina la baba na picha havikua vyangu kabisa.
RAMA; MAMA YENU AKIRUDI NAOMBA MUMUAMBIE KUWA MIMI NIMETOKA!---SEHEMU YA KUMI
Walinigomea kabisa kumchukua mtoto, mwanangu alikua akinililia na kutaka kuondoka na mimi, ili kuepusha aibu niliamua kumuacha mtoto. Hata rafiki yangu aliponiuliza nilimuambi hamna kitu. nilimchukua rafiki yangu na mwanaeo tukaondoka pale shuleni. Akili haikua pale kabisa, nilikua na mawazo mengi, nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa hata njia nilikua siioni vizuri.
“Vipi mbona hivyo?” Rafiki y angu aliniuliza.
“Hapana, hamna kitu nipo sawa sema kichwa naona kama kinaniuma, ghafla tu nasikia kizunguzungu. Hembu endesha gtari ni drop nyumbani, sijisikii vizuri kabisa.” Nilimuambia huku nikipaki gari pembeni, kwa namna nilivyokua ikijisikia nilijua naweza kudondosha gari, sikua sawa kabisa.
Alichukua gari na kuniacha nyumbani, kwakua yeye gari yake aliacha ofisini aliondoka na gari yangu. niliingia ndani mpaka chumbani, nikaingia kwenye kabati la mke wangu na kwenda kwenye briefcase yake moja ambayo alikua ameifunga, ni zile za kufunga na namba na kila siku nilikua nikiiheshimu, alikua hapendi niguse vitu vyake hivyo nilimheshimu kwani nilijua kama nikigusa inakua ni kelele na mimi huwa sipendi kugombana naye sana. Sikuhiyo sikujali chochote, nilishachoka na nilitaka kujua ukweli, nilijua kabisa kuwa kama nikifungua pakle nitakutana na kila kitu.
Nilitafuta kisu na kufungua huku nikiharibu kabisa ile sehemu ya kufungulia. Kulikua na document nyingi tu, nilianza kutafuta vyeti vya watoto. Kulikua na vyeti vya watoto vyakuzaliwa vitatu, vilikua original kabisa. Cha kwaza kilikua ni cha yule mtoto wake wakwanza ambaye mimi aliniambia kua ni mtoto wa mdogo wake. Cha pili kilikua ni cha mwanangu wa kwanza na chatatu kilikua ni cha mtoto wake ambaye alizaa kipindi aataka kuniacha. Cha ajabu vyote vilikua na majina ya yule Baba, hakuna hata kimoja kilikua na jina langu wala la yule kijana na vyote yeye ndiyo alikua Mama.
Nilishangaa kwakua cheti cha kuzaliwa cha mwanangu ambacho nacho kilikua ni original nilikua nacho mimi na cha yule mtoto wa pili nacho nilikua nacho na aliniandika mimi ingawa nilijua kabisa kuwa si mwanangu. Nilitafuta tafuta na kukuta tena cheti kingine cha mtoto wake wa tatu ambacho kilikua na jina la Baba la yule ambaye alitaka kuoana naye ikimaanisha kuwa huyo mtoto alikua na vyeti vtatu, vyote original ila kila kimoja na Baba yake. Nilikutana na hati mbili za nyumba ambazo zina jina lake, ni nyumba ambazo mimi nilikua sizijui na pia nilikuta cheti cha ndoa ambapo jina lilikua la yule mtu ambaye nilitajiwa mwanzo kuwa alishawahi kumuoa.
Niliishiwa pozi kabisa, kulikua na vitu vingine vingine lakini sikuvijali sana. Nilitaka kukaa kumsubiri mpaka arudi lakini nilishindwa, niliamua kwenda kumfuata dukani. Aliponiona alishangaa, alishanikataza kwenda dukani hivyo aliwaka sana na kuanza kuniambia niondoke.
“Leo nimeenda kumuangalia mtoto shuleni…” Nilimuambia.
“Mtoto? Mtotop gani?” Aliuliza huku bado akinisukuma ili niondoke. Sikuondoka, niliingia ndani na kukaa.
“Mtoto gani? Kwani una watoto wangapi wanasoma, nimeenda shuleni kwa mtoto wetu lakini cha ajabu nilitaka kumchukua nikaambiwa mimi si Baba yake?” Nilimuambia lakini hakuonekana kabisa kushtuka.
“Hayo ni mambo ya kuzugumzia nyumbai!” Aliongea huku bado akinisukuma, nilishangaa ni kwanini alikua hata hashituki.
“Mbona unaongea kirahisi namna hiyo, unajua kuwa nimeumia sana, nimeenda mpaka nyumbani kwenye begi lako nakuta vitu vya ajabu.”
“Begi langu? Hivi wewe una akili kweli, kwanii unaenda kupekua vitu vyangu? Umechukua nini? Hivi mimi nakaguaga vitu vyako, kwanini hukuja kuuliza kwanza kabla ya kuingilia mambo yangu! umenikara sana, ushaniharibia siku yangu!” Aliongea kwa hasira, sasa alionekana kupaniki kabisa aliposikia kuwa nimekagua vitu vyake. Alitoa simu yake na kupiga namba flani.
“Naomba usije leo, sisikiii vizuri naenda nyumbani.” Aliongea na mtu kwenye simu.
“Hapana siumwi! Sijisikii tu vizuri!” Aliendelea kuongea kwa asauti ya juu, walikua kama wanabishana.,
“Hapana, nsihakuambia huwezi kuja nyumbani kwangu, naishi na Mama yangu unafikiri Mama yangu akijua kuwa natembea na mume wa mtu! Nilishaambiwa nikuache mimi ndiyo king’anganizi, sitaki kumuua Mama yangu kwa mapresha yeye ni mtu wa dini! Nishasema usije, si umwi sana naenda tu kulala basi!” Aliongea kwa hasira na kukata simu, bila kujali kama nimesikia au la alianza kufuga duka, alikua akifunga huku akinilalamikia kwa kuingilia mambo yake, alitoka na kuingia kwenye gari, aliondoka na kuniacha pale.
Kwakuwa sikua na gari nilichukua bodaboda na kumfuata, tulifika pamoja, aliingia ndani moja kwa moja mpaka chumbani. Ile Briefcase niliyoipasua ilikua kitandani kila kitu nimemwaga chini, lakini hakuijali, aliingia kwenya kabati, akatoa nguo zaote, akatoa mbao flani kisha akatoa kabegi kadogo. Hako nilikua sijakaona, alikafungua na kuangalia vitu vilivyopo ndani na hapoa lipumua kidogo. Alirudisha ilipokua na kurudi kitandani, akaagalia vile vyeti na kuniuliza.
“Kwahiyo hivi ndiyo vimekupanikisha?” Aliongea hukua kicheka, ilikua ni kama kitu cha kawaida kwake, ni kama aliniona mpuuzi mimi kupaniki kwaajili ya kitu kama kile.
“Kwahiyo wewe unaona kama haya mambo ni mdogo? Kwanza una watoto wangapi? Lakini wakwangu ni yupi?”
“Maswali gani hayo sasa, wewe mwenyewe unajua nina watoto wawili, na unajua kuwa kitanda hakizai haramu, huyu mdogo si wako kweli lakini ulishanismahee kwakua hata wewe ulichepuka na una mtoto.” Aliniambia, nilimuuliza kuhusu vyeti na yule mtoto wa mdogo wake kutumia jina lake kama Mama.
“Hivi ni feki tu, hivi ni vyeti natumia kudanganyia wakati nikitaka pesa, unafikiri yule mzee angenijengea kama angejua sina mtoto wake. Hapa anajua nina watoto watatu wote wake lakini ukweli nikuwa hana hata mmoja, huyo mtoto wa mdogo wangu nilimuingiza tu ili apate mali zake, mzee ana pesa yule akifa tunatajirika.”
Aliendelea kuongea maneno ambayo sikumuelewa kabisa, mke wangu alikua anaongea kana kwamba kitu alichokifanya kilikua ni chakupongezwa, alijiona mjanja flani, nilimuangalia bila kummaliza.
“Watoto niwako na wewe ndiyo nakupenda, lakini siwezi kumaucha yule Baba kirahisi namna hiyo, nimetoka naye mbali, ameshanitumia sana hivyo na mimi lazima kumtumia, wewe unafikiri nikimuacha sasa hivi na akijua watoto si wake si ataniua. Mimi nimebadilika, kweli nakiri zamani nilikua sina akili nimefanya maujinga mengi lakini sasa hivi najielewa, najua nafanya nini, nakupenda wewe mume wangu lakini yule mzee nikimuacha ananiua, lazima niendelee kukaa naye kumdanganya danganya mpaka sukari imchukue basi!”
Mke wangu hakujali hisia zangu, aliongea kama kitu cha kawaida sana, nikiwa pale bado natakafakari sijui nini chakufanya alikusnaya vitu vyake, aliangalia nyaraka zake kama ziko sawa na kuondoka navyo. Alirudi jioni, mimi bado nilikua nyumbani, bado nilikua sijisikii vizuri na nilitamani kuongea naye ingawa hakuwa tayari kwa hilo.
“Mimi kesho naenda nyumbani, naenda kumuona Mama anaumwa.” Aliniambia, nilimuitikia tu sawa kwani nilikua na hasira sana, aliingia jikoni kuandaa chakula cha usiku lakini sikuweza hata kula, nilimuambia najisikia vibaya, aliishia kuniambia sawa kisha akaendelea na mambo yake, alikula na kurudi kupanga nguo, asubuhi aliondoka na kuniacha.
Mke wangu aliondoka na kuniacha na watoto wake wawili, mtoto wake wa kwanza ambaye alinidanganya ni wamdogo wake na yule wa tatu ambaye alizaa na mtu mwingine baada ya sisi kuoana. Mtoto ambaye wakati huo hata sikujua kama ni wangu au la alikua bweni anasoma. Nilikua na hasira sana hata kazini nilishindwa kwenda, nilikua najisikia vibaya kwani kila nilipokua nikimpigia mke wangu simu ilikua haipokelewi. Nilikua sijielewielewi, mpaka jioni nilikua sijatoka ndani na simu ya mke wangu ilikua haipokelewi, hasira zilinipanda. Nilimpigia simu Mama yake, baada ya salamu nilipotaka kuongea na mke wangu alijifanya network inasumbua na kukata simu.
Hapo hasira zilinipanda zaidi, nilijikuta naingia jikoni, nikachemsha maji mengi ya moto. Binti wa kazi alikua ashalala, ulikua ni usiku wa manane nilikua macho peke yangu. niliyaepua maji yale baada ya kuchemka sana nikayaweka kwenye ndooo, kisha ilitoka kuelekea chumbani kwa watoto.
“Hawa ndiyo wanampa kiburi ngoja niwaonyeshe!” Nilifungua mlango wa chumba cha watoto, bila kuwasha taa niliingia ndani, nikanyanyua ile ndoo huku nikielekezea kilipokua kitanda cha watoto niliyamwaga maji nusu kwenye kitanda kimoja nikageuka upande wapili na kumwaga maji ya moto nusu kwenye kitanda kingine ambacho kilikua na mtoto mwingine.
SOMA HAPA UPATE MESEJI NZURI ZA MAHABA
INAENDELEA

No comments