Header Ads

Header ADS

Simulizi: kijiji cha wachawi sehemu ya tisa (09)



Kwa kweli baada ya kuona mpenzi wangu nyamsale imemkolea sikuwa na jinsi. Niliamua nitulie tu kwanza huku nikiwa nawaza kitu cha maana ambacho ningefanya ili kuweza kukwepa kuwa mbwa. nilijua kuwa kukaa karibu na Yusira lazima ipo siku tutakuja kufanya tu mapenzi alafu baadae nakuwa mbwa kama maimuna alivyoniambia. Safari iliendelea hadi tulifika nyumbani kwetu. Kwa kweli mpenzi wangu maimuna yeye alionekana ni mtu mwenye furaha sana kwa ujio wa mdogo wake hali ambayo ilikuwa ipo tofauti sana na mimi maana nilionekana mtu ambae furaha ilikuwa imenitoweka kabisa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Baby mbona shemeji yako kaja unakuwa mpole hivi wakati wewe ndio wakumchangamkia shemeji na siyo mimi. Kwani kuna nini baby au unaumwa maana umepoa sana na siyo kawaida yako"Aliongea mpenzi wangu."Ni kweli mpenzi wangu kwa kweli leo mimi sipo vizuri kabsa. nashukuru kwa kuligundua hilo mapema maana kichwa kinaniuma sana. Tena bora mimi nikapumzike alafu naomba uniletee panado chumbani kwangu ninywe huenda nikapunguza maumivu"Nilimwambia mpenzi wangu huku nikiondoka kuelekea chumbani kwani hata hamu ya kukaa na Yusira nilikuwa sina kabsa. Nilimwambia Maimuna aniletee dawa chumbani kwangu makusudi ili niweze kupata muda wa kumueleza yote. yani muda ule nilishapanga kumwambia kila kitu mke wangu, Nilishapanga kumwambia hata ujio wa mdogo wake yusira ulikuwa siyo wa kawaida nyumbani kwetu. sikutaka kumficha tena ili kuweza kujiokoa mimi binafsi na penzi letu kwa Ujumla


******************************************




Baada ya kwenda chumbani kwangu nilijitupia kitandani na kulala huku nikiwaza mambo mbali mbali ambayo nilishawahi kupitia nyuma. yapo mambo ambayo nilikuwa nikikumbuka nacheka na yapo ambayo nilikuwa nikikumbuka huzuni unatawala moyoni mwangu. pia yalikuwepo mambo ambayo nikikumbuka mapigo ya moyo wangu yalikuwa yanaongeza kasi.




Baada ya kukaa kama dakika tano hivi chumbani kwangu nilisikia mlango ukifunguliwa. bila shaka nilijua ni mpenzi wangu Maimuna tu maana hakuna mtu yeyote ambae alikuwa anaingia chumbani kwangu bila kubisha hodi zaidi ya Maimuna.


ilibidi nigeuke kuangalia ili kulidhisha macho yangu ingawa moyoni tayari nilikuwa najua alikuwa maimuna. Nilipoangalia mlangoni nilikuta kweli alikuwa maimuna anaingia chumbani huku mkononi akiwa na glass ya maji.




Kitendo cha kumuona maimuna akiingia na glass ya maji chumbani kwangu kilinishitua kidogo maana maji ya kunywa hata chumbani yapo tena maimuna yeye mwenywe anayaweka. "Baby nimekuletea dawa unywe mpenzi wangu. pia pole sana najua utapona tu wala usiwe na wasiwasi"Aliongea maimuna huku akinipa ile glass ya maji. "Baby hivi umesahau kama kuna maji huku huku hadi umetoka na maji mlangoni au ndio NYAMSALE TENA"Nilimwambia mpenzi wangu huku tayari nilishapokea ile glass ya maji. "Najua kama kuna maji huku mpenzi wangu,lakini utamezaje dawa kwa maji baridi"aliongea mpenzi wangu huku akitabasamu hali iliyonifanya nigundue kuwa maimuna alikuwa ameongea ukweli. sikuwa na wasiwasi tena niliamini hakuna cha nyamsale tena yule alikuwa ni maimuna original.




"Baby kwa kweli mimi siumwi kichwa ila naumwa mawazo. na haya mawazo anayasababisha mdogo wako YUSIRA. Baby unajua mdogo wako ananitaka kimapenzi hata lengo la kuja huku alikuwa anataka tufanye mapenzi na mimi kitu ambacho mimi sitaki. Hata kipindi naondoka nilikuwa namkwepa Yusira kwani alishaniambia kwenye simu. hivyo tafadhari kwa kuchelewa kukwambia pia naomba mwambia mdogo wako kuwa mimi sitaki huo ujinga mimi nakupenda wewe tu"nilimwambia mpenzi wangu. Cha ajabu pamoja na kumwambia vile mpenzi wangu yeye wala hakukasirika zaidi ya kuanza kucheka hali iliyonishitua kidogo. ilibidi nimwangalie kwa makini kweli huyu ni maimuna au ndio mdogo wake. hata nilivyomuangalia vizuri ukweli ulibaki pale pale alikuwa maimuna. "baba sasa mbona nakwambia jambo la maana unanicheka. inamaana umeridhishwa na kile ambacho mdogo wako anakifanya"niliongea kwa hasira kidogo. "Kapopo bhana hivi unajua unaongea na nani"Aliongea maimuna maneno yaliyonifanya kushituka na kumuangalia tena usoni. cha ajabu nilipo mwangalia nilibaki nashangaa nilipoona alikuwa ni yusira.


CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kwa kweli ile hali ilinishitua sana,nilishindwa kuelewa imekuaje amekuwa Yusira ghafla wakati nilikuwa naongea na Maimuna. "Hivi unafikili kuna kitu chochote unaweza kumwambia Maimuna bila mimi kujua, acha kujidanganya Kapopo, kila unachokiwaza kumwambia Maimuna mimi nakijua. Yani mimi siwezi jua kile unachokiwa ambacha hakiniuhusu. Yani kitu chochote ambacho unataka kukiongea kinanihusu mimi lazima nijue. Ile ya kwanza si ilikuwa NYAMSALE sasa hii hapa ni BUGURA Yani nimemsahaulisha kile ulichomwambia Maimuna hivyo atakumbuka baada ya Nusu saa. Sasa nataka nikwambie kitu kimoja chamuhimu sana kwako kama unataka kuendelea kuishi. Sitaki umwambie kitu chochote maimuna kuhusu mapenzi yetu kama utamwambia tu kitu chochote kuhusu uhusiano wetu unakufa palepale. Kufanya mapenzi na wewe ni lazima maana ndicho ambacho kimenitoa Saud Arabia kuja Tanzania"Aliongea Yusira kisha alipotea ghafla. Kwa kweli yale maneno ya Yusira nae yalianza kuniweka wakati mgumu sana. Kule kwa Maimuna nimeambiwa kama nitafanya mapenzi na mwanamke yeyote yule lazima nigeuke kuwa mbwa alafu Yusira akaniambia kama nitamueleza Maimuna kuhusu kile ambacho Yusira amekiijia basi nitakufa. Nilishindwa nifanyaje maana ningemwambia Maimuna nilihisi ndio inaweza ikawa pona pona yangu. Nilikaa pale chumbani huku nikiwaza maana maisha Kwangu yalianza kuwa Magumu. Kwa mitihani ile ambayo ilinikabiri lazima nilijua naweza kufa au kugeuka Mbwa. Hapo ndio niligundua kumbe wanaofelly mashairiti wanapokuwa na mahusiano na jini siyo kwamba wanataka ila kuna vitu vingine vinatokea inakuwa vigumu kukwepa. Mimi muda ule yani nilikuwa najua kabsa nusu ya mwili wangu mbwa robo ya Mwili wangu nimekufa na robo nyingine ya Mwili wangu nilikuwa mzima. Muda ule uwezekano wa kuwa mbwa ulikuwa mkubwa maana Yusira alinihakikishia kuwa lazima nifanye mapenzi na yeye na nilipokumbuka kipindi kile Saudi Arabia ambae nilijikuta nilikuwa sitaki kufanya mapenzi alafu najikuta mzuka umenipanda ghafla ndio nilipata uhakika kama kuna uwezekano mkubwa wa kuwa mbwa. Kuhusu shariti la kufa kama alivyoniambia Yusira niliweka Robo tu maana nilikuwa na uwezo wa kuacha kumwambia Maimuna ila sikuwa na uwezo wa kumzuia Yusira kufanya mapenzi na mimi maana alikuwa anatumia nguvu za kijina zaidi. Kwa kweli muda ule nilikuwa na msongo wa mawazo hadi kichwa kilikuwa kinaniuma. Nilikaa chumbani kwangu hadi muda wa nusu saa tangia atoke Yusira ndipo mlango ulifunguliwa tena na Maimuna aliingia. "Mume wangu tafadhari naomba unisamehe si nilishasahau kama uliniambia nikuletee dawa uje kunywa. Yani isingekuwa Shemeji yako kanikumbusha hadi sasa ningekuwa sijakuletea. Na wewe unashindwa hata kuja kunikumbushia baby. Alafu unajua nashangaa sana siyo kawaida yangu hata siku moja kusahau kufanya kitu sijui leo kuna nini"Aliongea mpenzi wangu huku akinipa maji na dawa ninywe. Nilimwambia mpenzi wangu wala asiwe na wasiwasi maana nilijua BUGURA ndio ilimfanya hadi asahau. Kwa kuwa Muda ule kichwa nacho kilikuwa kinaniuma kwa ajili ya Mawazo basi niliamua tu kunywa zile panado. Nilitamani kumwambia Maimuna pale pale kitu ambacho Yusira alikijia lakini upande mwingine wa moyo wangu ulikuwa unaogopa kufa kabsa. "Mpenzi wangu kwa kweli nakupenda sana, wewe ndio kila kitu kwangu. Kama siku utakuja kuona nimefanya kitu kibaya juu yako naomba uje unisamehe. Ipo siku tu najua tutakuja kukosana na wewe ila naomba usije ukaniadhibu kama ulivyowahi kuniambia. Nahitaji uje unipe muda kidogo nikueleze kile ambacho kilifanya labda hicho kitu kitokee. Maimuna sasa hivi kwa kweli upo peke yako tu kwenye moyo wangu. Pia baby sasa hivi nataka niwe na wewe kila sehemu. Yani nataka hata bafuni kuoga tuwe tunaoga wote, kazini tunaenda wote yani kila sehemu"Nilimwambia Maimuna huku hadi machozi yakinilenga lenga. Kama kumwambia Maimuna kile ambacho Yusira alikiijia ningekufa basi muda ule niliamua kila mahali ningekua naye. Hiyo ndio njia nilihisi inaweza kunikomboa ingawa nilikuwa sina uhakika. "Duuh Haya baby wangu chochote wewe unachotaka mimi nipo tayari hata ukitaka uwe unanisindikiza hadi chooni its okey. Hata mimi nakupenda sana mpenzi wangu ndio maana nahakikisha nafanya kila kitu ambacho wewe kitakupendezesha. Ila kama kuna kitu chochote kinakufanya usiwe na furaha niambie mimi nitakifanyia kazi"Aliongea Maimuna




Kwa kweli yale Maneno ya Maimuna kunielewa kile ambacho nilikuwa nimemwambia kilinifurahisha sana. Nilitamani kumueleza Maimuna kuhusu Ujio wa Mdogo wake ila moyo ulisita kabsa. Sikuwa tayari kufa na kumuacha Maimuna duniani peke yake wakati bado moyo wangu ulikuwa unampenda sana. Niliamua kukaa na ile siri vile vile kama Yusira atakuja kweli kunilazimisha kufanya mapenzi nilipanga kukataa na kumuelezea mashariti ambayo Maimuna aliniambia ya kuwa Mbwa kama nitakuja kufanya mapenzi na Mwanamke yeyote yule. Pia kuwa karibu na Maimuna Muda wote nilihisi ingekuwa vigumu kwa Yusira kuweza kufanikisha lile lengo lake ambalo alikuwa analitaka. Baada ya Maongezi ya hapa na pale na Maimuna Tuliondoka wote na Maimuna kuelekea Mlangoni kwenda kupiga Stori na shemeji yangu Fake. Namuita shemeji yangu Fake kwa kuwa yeye alikuwa ananitaka kimapenzi wakati anajua kabsa kama ninauhusiano na dada yake. Tulipofika Mlangoni tulikuta Yusira yupo tena Uzuri zaidi alikuwa yupo na baba yake. Nilipomuona baba yake na Maimuna kwa kweli akili ilinituma kumueleza yeye. Nilihisi baba yao anaweza kuwa Msaada mkubwa kwangu. "Daah Wanangu yani sasa hivi hamtaki kabsa kwangu kunitembelea. Hivi sasa hivi kisiwani mmepasahau kabsa mmenogewa na hii dunia. Mnatakiwa mkumbuke huko Kisiwani ndio kwenu mje mtuangalie hali yetu. Mwanangu kapopo wewe sasa hivi kisiwani ni kwako kabsa. Unatakiwa uwe unakuja kututembelea Mwanangu ili uweze kujua mambo mbali mbali ambayo yanafanyika kule kisiwani. Kwanza nashangaa Wanangu mmeganda huku wakati Maisha ya Raha yanapatikana KISIWA CHA MAJINI. Alafu wewe Maimuna naomba uwe unamleta Mkwe wangu kisiwani kama wewe umepachoka basi nahitaji mwanangu uwe unamleta"Aliongea baba yake na Maimuna. Yale maneno ya Mzee kwa kweli yalinifurahisha sana. Yule baba yake na Maimuna kwa kweli alikuwa ananipenda ile mbaya. Sijui kwa nini yule mzee wa kijini alikuwa ananipenda vile. Pia yule mzee kwa kweli ingawa alikuwa mzee lakini bado alioneka mzee hand some kweli. Yani hata nilipokuwa namuona nilikuwa namwangalia mara mbili mbili. Jinsi alivyokuwa anavaa na kupendeza hadi ilikuwa raha kumuangalia"Basi baba usiwe na wasiwasi mimi kila Juma mosi nitakuwa namleta huko tunakaa hadi siku ya Juma tatu ndio tunarudi huku Duniani. Ila baba hata mimi nakaribia kukuletea Mjukuu wa binadamu mwingine tena. Wewe si unapenda sana binadamu basi mimi sasa hivi mjamzito na nakuletea Mjukuu "Aliongea Maimuna. "Hongera sana Mwanangu, pia hongera Sana kapopo kwa kukaribia kuniletea mjukuu wangu wa kwanza. Kwa kweli hicho ndio kilikuwa kilio changu kuweza kupata mjukuu kabla ya kufa kwangu maana hadi sasa nilikuwa sina Mjukuu kabsa. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Tena mimi naondoka na Kapopo sasa hivi kwenda kisiwani kumpatia zawadi yake. Ila Maimuna Mwanangu kuwa Makini kwani siku kama hizi ndio mambo Mengi huwa yanaharibika. Kwa kweli nimeshuhudia Ndoa nyingi za mabinti wa kijini wanapoolewa na binadamu huwa zinaharibikia hapa. Unatakiwa kuwa Makini sana siku hizi za Ujauzito wako ili usije kuharibika"Aliongea Baba yake na Maimuna huku akiwa na Furaha mbaya. Kwa kweli mimi nilibaki nikiwa nashangaa tu maana kwa sisi binadamu huwa siyo kawaida binti wa kike kumwambia baba yake kuwa anamimba ila kwa Majini ilionekana kawaida sana. Pia nilifurahia Sana baba yake na Maimuna aliponiambia kuwa tutaenda kisiwani Pamoja maana nilipanga ndio Muda Mwafaka wa kumwambia kuhusu Yusira anavyonisumbua. "Baba Usiwe na Wasiwasi nitakuwa makini sana kipindi hiki na kuhakikisha nakupatia mjukuu. Pia mimi nakuruhusu Ondoka na Kapopo ila naomba asipitishe siku mbili huko maana natamani sana kuwa karibu na mume wangu"Aliongea Maimuna. Yale maneno ya Maimuna ndio yalizidi kufanya nimpende zaidi. Yani Muda ule kuishi na Majini nilikuwa naona rahisi sana, ila Yusira ndio Jini ambae alikuwa ananifanya kukosa raha. Isingekuwa Yusira kwa kweli Maisha ya kuishi na Majini kwangu nilianza kuona mazuri na yalikuwa yakawaida tu. Baada ya Maongezi ya hapa na pale ndio mzee aliwaaga wanae na kuniita mimi tuondoke kuelekea Kisiwani. Nakumbuka hiyo Siku kwa kweli tuliondoka kimaajabu sana maana Hatukuenda kwenye kioo kama nilivyozea kwenda. Baba yake na Maimuna aliniita tu nikaenda hadi sehemu ambayo alikuwa Amesimama. Alichofanya aliweka mkono wake kichwani kwangu akaniambia nifumbe macho kisha kuongea Maneno ambayo yalikuwa Mageni sana kwangu. Alipomaliza kuongea yale maneno alitulia kama dakika moja alafu baadae aliniambia Fumbua macho. Nilipofumbua Macho kwa kweli nilijikuta nipo Nyumbani kwa baba yake na Maimuna. Tena nilimkuta mzee ameanza kunywa na kahawa kabsa.




Kwa kweli ile njia ya kusafiri kwa yule Mzee kurudi home kwake kwa kutumia ile nyumba kwangu ndio kilikuwa kitu cha ajabu sana. Tangia niwe na uhusiano na Jini sikuwahi kuhisi kama kuna usafiri wa namna ile. Bora wa ule wa Maimuna wa kutumia kioo au unapoteza fahamu ila siyo wa huyu mzee ambae unakuwa Macho alafu ndani ya sekunde unajikuta sehemu nyingine kupitia ile nyumba. "Kunywa kahawa Mwanangu tena nimepata taarifa tayari Kina Maimuna na Yusira wameshaingia kisiwani na tayari wanaelekea kwenye ukumbi wa Kufanyia Sherehe ya Yusira. Hivyo wahi kunywa kahawa ili tuweze kwenda tukamalize mambo yetu pamoja na lile la kukukabidhi pesa"Aliiongea Baba yake na Maimuna maneno ambayo yalinishangaza sana. Maana wakati tunatoka duniani ilikuwa bado siku tatu za kufanya ile sherehe ya Yusira lakini huku nimefika hata saa tatu sijamaliza Naambiwe tena tukafanye sherehe ya Yusira. "Haina Shida Mzee wangu nakunywa kahawa. Ila hata hivyo mzee wangu Kuna kitu bado kinanitatiza. Unakumbuka wakati tunatoka Duniani uliniambia kuwa sherehe ya Yusira itafanyika baada ya siku tatu sasa mbona hata saa tatu hatujamaliza unaniambia Yusira na Maimuna wameingia kisiwani na tunatakiwa tuelekee kwenye sehemu ya kufanyia sherehe mbona hii mimi bado haijanikaa akilini" Nilimwambia Baba yake na Maimuna maana uvumilivu ulinishinda. "Unajua kapopo kwanza unatakiwa ukumbuke kutoka Duniani hadi kuja huku kisiwani ni mbali sana. Kwa mfano labda kama Kungelikuwa tunasafiri na Gari basi tungekuwa tunatumia zaidi ya wiki moja ndio unafika. Yani unatakiwa uelewe haya mambo tunayapeleka kijini zaidi. Yani kutoka Duniani hadi kufika huku kisiwani kwa Usafiri wa Kijini zaidi tumetumia siku tatu. Ila sema wewe binadamu huwezi ona ila mimi jini ndio ninauwezo wa kuona. Yani kipindi Yusira amefika wote tayari mlikuwa mpo safirini kijini zaidi kufika huku ila sema wewe huwezi kuhisi hata siku moja. Utaendelea kujiona upo mazingira ya nyumbani tu lakini kumbe upo safarini. Pale tu nilipokugusa kichwani ndio ulikuwa umefika kisiwani ndio maana unashitukia paa upo kisiwani. Hivyo kuelewa haya mambo kwa wewe binadamu ni vugumu sana. Ila unatakiwa uelewe tayari siku tatu zimeisha na tunatakiwa kwenda kwenye sherehe ya Shemeji yako"Aliongea baba yake na Maimuna maneno yaliyoniacha nibaki nikiwa nashangaa tu. Sikutaka kumuuliza swali lolote maana majibu ambayo nilikuwa nayapata kama nilihisi yananichanganya kichwa changu tu. Nilikunywa Pale kahawa hadi tulimaliza kisha tulitoka nje ya nyumba ili tuanze safari yetu. Tulipotoka nje ya nyumba nako nilibaki nikiwa nashangaa nilipoiona ile gari ambayo tulikuwa tumepaki kwenye ile nyumba ya ajabu na yenyewe ipo pale ndani. "Kwa kweli Jini siyo kitu cha kuchezewa hata kidogo, inamaana hata gari limesafirishwa na ile nyumba limekuja hadi nyumbani kwa huyu mzee" nilijisemea kimoyo moyo huku nikiwa nashangaa maana Gari nakumbuka tulikuwa tumeliacha kwenye ile nyumba kabsa. "Ndio hivyo Mwanangu hata Gari inasafirishwa kuja hadi nyumbani kwangu maana Kila Gari inausajili wa nyumba yako. Mfano ukiangalia namba ya gari yangu alafu ukaangalia na namba ya nyumba yangu utakuta zinafanana"Alinijibu baba yake na Maimuna hali iliyonifanya kushangaa zaidi maana yale maneno ambayo alinijibu mimi nilikuwa najiuliza kimoyomoyo wala sikutamka hata neno moja. Sikutaka kumuuliza amejuaje kama nilikuwa najiuliza kitu kile kichwani Mwangu. Tulienda tukapanda kwenye ile Gari na Safari ya kuelekea kwenye ukumbi wa sherehe ambae sikujua upo wapi ilianza. Gari ilikimbia kama muda wa dakika kumi na moja hivi kisha Ghafla nilishangaa tunatokezea juu ya bahari huku gari ikiwa inakimbia bila kuzama. Kilichozidi kunishangaza zaidi kweli Gari yetu ilikuwa ipo juu ya bahari na inakimbia lakini hakuna maji ambayo yalikuwa yanatwanyika tairi zilipokuwa zinapita wala Gari kuzama zaidi nilikuwa naona kwa nyuma kitu kama vumbi hivi linatimka. Gari ilikimbia hadi tulipokaribia sehemu ambayo niliona Magari mengi yakiwa yamepaki kuzunguka jengo zuri ambalo nalo lilikuwa limezungukwa na Maji. Hata yale Magari yalikuwepo majini. Tulipofikia yale Gari baba yake na Maimuna alisimamisha na kushuka kwenye yale maji bila shida. Mimi pia nilifata na kushuka. Ile nimekanyaga tu yale maji nilishangaa sikuona maji tena zaidi niliona nchi kavu tena kuna vumbi alafu ilionekana nipo kwenye kisiwa ambacho kilikuwa kimezungukwa na maji pande zote. Tuliingia hadi Ndani ya lile jengo na kukuta watu wakiwa wengi sana. Nilipoingia kwenye lile Jengo nilibaini ilikuwa ni lile Jengo ambae nilifungia ndoa na Maimuna. Nilipoangalia mbele ambapo walikuwa wamekaa watu wakubwa nilishangaa kuwaona wazazi wangu wote wawili mama yangu na baba yangu na wenyewe wapo kwenye hiyo sherehe-




CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kwa kweli nilipowaona wazazi wangu nilishituka kidogo maana sikutegemea kama watakuwepo kwenye ile Sherehe. Hata mama yangu ambaye ndio nilimtoa kafala kama mahali ya kumuoa Maimuna alikuwepo. Muda ule tangia maimuna anionyeshe sikuwa nafatilia tena kuhusu kujua mama yangu amekufa kweli au mzima hata nilipomuona Mama yangu wala sikushituka sana. Pale mbele pia kulikuwepo Maimuna na Yusira ambae walikuwa wamekaa pamoja. Pia kulikuwepo na mtu ambae hakuwa binadamu wa kawaida kabsa. Yule mtu kweli usoni alikuwa na sura ya binadamu ila baadhi ya sehemu zake za Mwili zilikuwa zinaonekana tofauti. Yule mtu kwanza alikuwa na Masikio Marefu kama ya Farasi huku nyuma akiwa na mkia na miguu yake ilikuwa haina utofauti na Punda. Nilipomuona yule mtu yani hata sikushituka maana yale mambo muda ule nilishayazoea sana. Upande wa Mwisho katika vile viti nilimuona na Rafiki yangu Mdete alikuwepo, hata nilipomuangalia alikuwa mtu mwenye furaha sana na Muda wote alikuwa anatabasamu. Nilichoamua kabla ya kukaa ni kumfuata mdete ili kwenda kumuuliza ili kujua anajua kama tupo Kisiwa cha majini. "Mdete kuna Rafiki yangu Maulidi anaulizia tupo Ukumbigani ili aweze kuja kwenye hii Sherehe. Unajua mimi si nilipakiwa kwenye gari yenye vioo vya tinted sasa sikuweza hata kujua huu ni Ukumbi gani"Nilimuuliza Mdete lengo kutaka kujua yeye anajua tupo Ukumbi gani. "Rafiki yangu kweli sasa hivi mambo yamekubana hadi kumbi unanizisahau. Kumbi ambayo tulikuwa wapenzi wa kuja kuangalia Fiestar leo hii umeisahau kabsa. Mwambie tupo Singida hotel au kama vipi mpigie simu mimi nikamchukue na Gari chap" Alinijibu mdete maneno ambayo yalinifanya kubaki nikiwa natabasamu huku nikiwa namshangaa. Ule ukumbi ambao sherehe ilikuwa inafanyikia kwanza Singida nzima ilikuwa hakuna wala sikuwahi hata kufikilia kama singida kunaweza kukaja kuwa na ukumbi kama ule. Ule Ukumbi uzuri wake naweza kulinganisha Na ukumbi wa Bunge ila kimuundo ulikuwa upo tofauti na ule ukumbi ulikuwa mzuri kuliko hata Wa bunge. Sasa kitendo cha Mdete kuniambia kuwa tupo Ukumbi wa Singida hotel kiliniacha mdomo wazi. Sikutaka kumshangaa sana hali ambayo ingemfanya Mdete kunisoma maana ni yeye tu ambae alikuwa na taarifa juu ya mimi kuwa na mke jini. Hivyo kama ningejifanya kushangaa sana lazima Mdete angenisoma. Nakumbuka Baba yake na Maimu aliniambia kuwa wakati tunakuja huku Kisiwa cha Majini huwa tunatumia muda Wa siku mbili hivi. Yani binadamu huwa anakuwa Safarini bila kujiona. Kitu ambacho nilikuwa nimekifanya kwa Muda ule ni kujaribu kumtafuta rafiki yangu Maulidi kisha namwambia Mdete akamchukue. Kama Mdete ataenda na kutumia siku mbili zaidi ndipo ningeamini yale maneno. Pia nilitaka kujua Mdete anagetokaje pale na Kusafiri maana lile Jengo lilikuwa limezungukwa na Maji kila Upande. Nilichofanya nilienda kwenye meza yangu na kukaa. Mimi nilikuwa nimekaa kiti cha mbele huku kwa nyumba yangu alikuwa amekaa shemeji yangu Yusira. Sherehe ilianza Rasmi huku ikianza kwa Utambulisho wa Pande mbili. Hata ilipofika zamu ya mama yangu kujitambulisha alijitambulisha tu kama kawaida tena kwa Jina lake. Hapo kwa kweli nilihisi Mama yangu bado alikuwa yupo mzim ila sema kuna kitu nilikuwa nafichwa tu na Maimuna. Baada ya utambulisho kupita nilimpigia Simu Maulidi na kumwambia kuna sherehe nafanya Singida hotel hivyo Mdete atakuja kumchukua. Maulid alikubali na nilienda hadi kwa Mdete kwenda kumtaarifu kuwa anatakiwa kumfuata Maulidi. Baada ya kumpa ile taarifa Mdete aliondoka na kutoka nje kwenda kumchukua Maulidi. Baada kama Muda wa Robo saa kupita nilishangaa kumuona Mdete wakiingia na Maulidi. Kwa kweli ile hali ilinifanya kubaki nikiwa nashangaa na kutokuelewa kabsa hii inakuwaje. Niliamua kutulia jibu langu nilijua nitalipata kwa Baba Maimuna. "Kwa kweli katika siku ambazo nimekuwa na Furaha ni hii siku ya leo. Tayari hadi sana nimempata Mrithi wangu wa mali wa kiume pia ni sherehe ya mtoto wangu Yusira. Hii ilikuwa ni sherehe ya Mwanangu Yusira kumkaribisha tena kwetu maana tangia aende Saudi arabia anasiku nyingi hajarudi nyumbani. Ila kupitia hihi sherehe na mimi nitamtangaza Mrithi wa Mali zangu. Yeye ndio atakuwa Nguzo yangu ya familia na atakuwa na mamlaka ya kumiliki mali zote za familia yangu. Hii nikiwa na maana kuanzia sasa mwanafamilia ukiwa na shida ya pesa hautanifuata mimi bali utamfuata huyu ambae nitamtaja. Hata mimi sasa hivi nikiwa na shida ya pesa itabidi nimuombe huyu ambae nitamkabidhi. Ambae atakuwa Mrithi wa Hizi mali si Mwingine ni Mkwe wangu Kapopo bin Omari"Aliongea baba yake na Maimuna na watu wote waliitikia kwa kupiga makofi na vigelegele. Ukumbini mle kulikuwa kumetapakaa watu wenye sura nzuri sana ambazo zilikuwa zinavutiwa sana. Yani mtu mmoja tu ndio ambae alikuwa na Sura ya kutisha. Wakati watu wakiwa wanaendelea kupiga vigelele kwenye miguu wangu chini ya kiti nilihisi kama kitu kinanipapasa. Nilipochungulia kuangalia ulikuwa mguu na wani nilikutana na Mguu wa Yusira. Niligeuka kwa hasira ili kumwambia kwa nini anafanya hivyo tena tupo mbele za watu. Cha ajabu ambacho hadi sasa huwa bado kinanishanga nilipogeuka kwa hasira nilishangaa hasira yangu yote inapotea ghafla hata linipomgeukia nilitabasamu tu kama vile nimefurahishwa na kile kitendo. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/






Kwa kweli ile hali ilikuwa inanishangaza kweli kila nilipokuwa nageuka kwa Yusira hasira zangu zilikuwa zinayeyuka ghafla na kutabasamu huku nikifulahia kile kitendo. Nikigeuka kurudi ile sehemu ambayo nilikuwepo nilikuwa napandwa na hasira sana hadi kutamani kuukata mguu wa Yusira. Sikuwa na jinsi wala kadeki niliamua kutulia tu huku hasira zikijikusanya na kumuacha Yusira kuendelea na kile kitu ambacho alikuwa anakifanya. "Huna haja ya kukasilika kapopo chamuhimu kila ninachokifanya unatakiwa ukubaliane nayo tu. Hii stairi ya kunigeukia unajikuta upo kwenye furaha badala ya chuki inaitwa KINKUMBA. Najivunia kuzaliwa jini mwenye uwezo mkubwa sana hivyo huna jinsi kama mapenzi tutafanya sana"yalikuwa ni maneno ya Maimuna ambayo aliniambia baada ya kusogea karibu kabsa na sikio langu. Yale maneno kwa kweli yalinifanya kupoteza hata Mzuka wa ile sherehe na kujikuta natokwa na Machozi. Nilijua hichi ambacho Maimuna anataka kukifanya kitanishushia heshima yangu kwenye huu ukoo wa majini kitu ambacho nilikuwa sitaki kabisa. Tena nisingeshushiwa heshima tu pili ningeweza kuwa mbwa kabsa kama maimuna ambae alishawahi kuniambia kama nikifanya mapenzi na mwanamke yeyote basi nageuka mbwa. "Baby unacheka nini wakati tupo mbele na kunawatu wakubwa unafikilia watakuchukuliaje"Nilimsikia Maimuna akiniambia hali iliyonifanya kunyamaza ghafla kulia. Yani mtu nilikuwa nalia leo hii Maimuna anaona nacheka. Kwa kweli Yusira hakuwa Mtu mzuri hata siku moja. Baada ya sherehe kuisha watu walianza kupata chakula mbalimbali. Huku na Mimi tukiwa tunakula meza moja mimi maimuna na shemeji yangu Yusira. "Yusira huyu ambae amekaa kwenye hiki kiti kizuri kuliko vyote ni nani, maana anaonekana ni mtu mkubwa lakini nashangaa wala hajaongea kitu chochote"Nilimuuliza Yusira huku tukiwa tunaendelea kula Maana yule mtu alionekana mtu mwenye wadhifa wa Juu sana. "Huyo hapo ndio kiongozi Mkuu wa Majini yote, huyo hawezi kuongea Maana tayari alishakufa na pale ni mzimu wake wa jini ambae huwa unauhudhulia sherehe mbalimbali za kijini. Yani Sisi Majini Jini yeyote akifa kama bado majini wanamuhitaji huenda alikuwa kiongozi mzuri wa majini mzimu wake huwa unarudi na kuendelea kufanya kazi kama kawaida ila huwa hauna uwezo wa kuongea wala kula wenyewe unasikiliza na kufanyia mambo mbalimbali kazi ambayo yameongelewa pale"Alinijibu yusira majibu ambayo yalinifanya nizidi kushangaa sana. Kumbe ndio maana yule mzee alikuwa yupo kimya huku akiwa anaangalia hata chakula wakati sisi tunakula yeye hakuwa anakula. "Unajua Yusira kipindi nikiwa na mzee kuna mambo mengi sana kanifundisha na kuniambia. Katika Jambo ambalo limenishangaza ni jinsi ilivyo mbali kutoka Duniani hadi huku kisiwa cha majini. Mzee aliniambia kuwa huwa tunatumia siku zaidi ya mbili kusafiri. Yani mimi binadamu wa kawaida wakati nikiwa nasafiri huwa siwezi kuona na nyinyi majini mnaona. Nikifika Kisiwani nashitukia ghafla tu nipo kisiwani baada ya kunifanyia mambo yenu ya kijini kama kuniwekea mkono kichwani kama alivyofanya baba yako au kupitiwa na usingizi wa ghafla. Hicho mimi nilikielewa sana ila nataka kujua kama kutoka duniani hadi kisiwani tunatumia siku mbili huyu Rafiki yangu Maulid alifikaje huku kisiwani maana nilifanya maamuzi papo kwa papo baada ya mdete kusema amfuate"Nilimwambia Yusira Maneno ambayo yalimfanya Maimuna kuanza kucheka. Maimuna alipotabasamu na kufumbua mdomo wake na sauti ya kicheko kutoka kwa kweli alizidi kuwa mzuri ile mbaya. Ile hali kwa kweli ilinifanya kujisikia raha sana maana Maimuna nilikuwa nampenda mbaya . "Yani wewe kapopo unatuchezea sana sisi majini, unajua sisi majini tunauwezo wa kujua vitu vyote ambavyo utakuja kuvifanya ukiwa mahali flani. Kuna Utaalamu unaitwa MSULI LENGE huo ndio unatufanya sisi kujua kitu ambacho wewe utakuja kuvifanya ukiwa sehemu flani. Ndio maana kabla ya wewe kufika hapa tulijua utakuja kushangaa kumuona Mdete pia utaagiza maulidi kuja hivyo Maulid nae alikuwa kwenye safari ya siku mbili kitambo na tayari alikuwa yupo kisiwani bila yeye kujitambua. Tunachofanya sisi binadamu ambae hatutaki wajue mzingira ya kisiwani kama mdete maulidi na wazazi wako huwa tunabadilisha tu mazingira ya kisiwani yanaanza kuonekana kama mazingira ya sehemu hiyo walipo wahusika. Mfano sasa hivi binadamu wote ambao wapo kwenye hii sherehe wanajua wapo Singida motel kumbe wapo KISIWA CHA MAJINI"Aliongea Yusira wa undani zaidi hali ilyonifanya kukosa neno la kuongea na kukubali kama majini ni chama Jingine. Sayansi ya majini ilikuwa imekamilika sana kama na sisi bindamu tungekuwa na uwezo wa kufanya hivyo tungekuwa tupo juuu sana




Kwa kweli yale Maelezo ya Yusira yalizidi kunishangaza sana. Kintendo cha Jini kujua mawazo ya binadamu ambayo anayafikilia kabla ya tukio kufanyika ilikuwa siyo kitu cha kawaida. Nilikumbuka hata Mdete aliniambia kuwa tupo Ukumbini wa Singida Motel hivyo ambacho alikiongea Yusira kilikuwa kipo Sahihi. Sikuwa na Neno la kuulizia tena Zaidi nilikaa na kuendelea kula. Baada ya Muda kama wa Nusu saa hivi tayari binadamu wote na Majini ambae walikuwa kwenye ile sherehe yetu walikuwa wameshamaliza kula. "Tunatakiwa tusimame wote ndugu zangu ili kuweza kumuaga Mgeni maana ni Muda wake wa kuondoka"Aliongea Rijirafu baba yake na Maimuna. Watu wote walisimama na mimi nilisimama ili kumuona mgeni gani anaondoka. Bado nilikuwa na utata kati ya Yusira na yule mzee ambaeCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/ niliambiwa mzimu wa kijini nani ambae alitakiwa kuondoka maana wote ndio walikuwa watu wakubwa kwenye ile sherehe pamoja. Baada ya kuhakikisha watu wote wameamka ndipo nilimuona yule mzee akilala kwenye kiti ambacho alikuwa amekalia na kupotea kwa ghafla huku ikifatia na kishindo cha kutisha. Ambacho kilizidi kunishangaza ile style ambayo alipotea yule Mzee nilikuwa nashangaa mimi tu kwani Nilimuona Mdete na Maulid Pamoja na binadamu wengine wakiwa wanapiga makofi kama inshara ya kumpongeza yule Mzee alivyopotea. Ile hali kwa kweli Upande wangu ilinitia wasiwasi na kujiuliza Maswali mengi inamaana hawa watu walikuwa hawajaona tukio ambalo lilikuwa linaendelea. Ilibidi na Mimi nilianza kupiga tu makofi huku nikiwa natoka kwenye kiti ambacho nilikuwa nimesimama karibu nacho na kuanza kutembea kuelekea kwa Mdete. Lengo langu nilitaka kwanza kwenda kumuuliza Mdete huyu mtu ambaye amepotea na wanampigia Makofi anamjua pili nilitaka kuelewa je anajua kama huyu mtu kapotea ghafla au vipi. Kutoka sehemu ambayo nilikuwanimekaa hadi kwa Mdete ilikuwa siyo mbali sana Maana ilikuwa kama umbali wa mita tano tu hivi. "Mbona unapiga sana Makofi, inamaana unataka kuniambia huyu mtu ambae anatoka unamfahamu sana au"Nilimuuliza Mdete kichokozi ili ajibu. "Jamani Kapopo mbona unazidi kuwa Punguani hivi. Inamaana unataka kuniambia hata Mkuu wako wa Mkoa humjui. Unataka Kuniambia Josephina Chauzee Umemsahau. Huyu si ndio aliwahi hata kuja kwenye Mahafili ya kidato cha nne na kuchangia laki tano kwa ajili ya michezo. Hebu Jaribu kumuangalia vizuri si hajatoka ndio huyo anatembea kuelelea Nje. Alafu huyu mama hutuba zake zipo vizuri sana hivi umeona Jinsi alivyokua anaongea Maneno yake yani utazani yamepangilia na Compyuter. Anaongea Ponit tu huyu mama kweli kichwa"Aliongea Mdete na kuzidi kupiga Makofi. Kwa kweli nilibaki nikiwa namshangaa mdete maana majibu ambayo alinipa hadi nilihisi labda Jamaa kawa chizi nini. Ilibidi niangalie tena kwenye ule Ukumbi kama nitamuona yule mtu ambaye Mdete alikuwa Anamzungumzia lakini hakuna ambacho nilikiona. Mimi nilivyokuwa Najua ule mzimu tangia uingie pale Ukumbini haujaongea kitu chochote hata yusira aliniambia vile sasa mdete kuniambia Hutuba ya yule mgeni aliyetoka ilikuwa nzuri ndio nilichoka zaidi. Nilijua tu hizi zote ni Mbinu za kijini hivyo sikutaka kubishina na Mdete zaidi"Sawa nimemfahamu unajua hata mimi nilikuwa namfananisha ndio maana nilikuja kukuulizia kimtego ili nimkumbuke"Nilimwambia Mdete huku nikiendelea kupiga Makofi na kurudi kwenye kiti ambacho nilikuwa nimekaa. Nilipofika hapo nilishangaa Kuwaona Yusira na Maimuna wakiwa wananicheka mbaya. Mimi sikutaka kuwauliza kitu chochote zaidi ya kutulia. Baada ya Muda tena Mzee Hijirafu alisimama na kufunga sherehe kisha aliruhusu watu waanze kutoka maana tayari sherehe ilikuwa imemalizika. Watu wote walianza kutoka ila cha ajabu hakuna hata binadamu mmoja ambae alikuja kuniaga. Hata rafiki yangu mdete sikuwa Namuona tena. Baada ya watu wote kutoka hatimae na mimi nilitoka na yule mzee Hijirafu hadi nje tukapanda kwenye gari na kuondoka




Wakati wa kuondoka na Baba yake na Peninna Mzee Hijirafu sikuwa naona kabsa Maji ambayo Mwanzo wakati tunakuja kwenye Ukumbi nilikuwa naona Maji. Muda ule nilikuwa naona barabara ya kawaida tu wala hakukuwa na maji tena. Uzuri kila kitu ambacho nilikuwa nakiona Muda ule nilikuwa sishangai maana nilikuwa naona kawaida sana. "Mwanangu sasa ndio unaenda kuanza kuona Uzuri wa kuwa mkwe wangu. Kwa kweli Mwanangu ushindwe mwenyewe sasa kutumia pesa na Utajua Mwenyewe utafungua biashara gani Kubwa ambae itakufanya Ufahamike Afrika mashiriki nzima ikiwezekana hata Duniani. Unajua nakwambia hivyo kwa Sababu hatua ambayo umepiga Mwanangu ni kubwa sana na unauwezo wa kuwa mtu kumbwa na tajiri wa kupindukia hapa Tanzania. Kitendo cha kufikia kukukabidhi mali za kijini na wewe kuwa mmiliki siyo kitu cha mchezo. Nafanya hivi kwa kuwa Nakupenda Mwanangu tena nakupenda sana. Najua Muda umekaribia wa kuniletea Mjukuu wangu wa kibinadamu hivyo unatakiwa kuwa makini zaidi muda huu. Nakuomba jitaidi kufuata vitu vyote ambavyo nakwambia hususani kutokukufanya Mapenzi na Mwanamke yeyote hapa Duniani. Kama Utasubutu kufanya hivyo basi Utamua mtoto wako tumboni kwa Mwanangu Maimuna na kunifanya mimi kukosa mjukuu. Siyo Mimi kukosa Wajukuu tu hata wewe nitakukosa kwa kuwa tayari utakuwa Mchafu ambae hautakubarika tena katika koo za Majini. Unajua nakujali sana Mwanangu ndio maana nafikia kukwambia Mambo ambayo mtu kama Mkwe hapaswi kukwambia"Aliniambia Mzee Hijirafu kwa Utulivu wa hali ya Juu. Kwa kweli yale Maneno ya yule Mzee kama ndio yalizidi kuniumiza zaidi maana nilikuwa natamani sana kutimiza kila kitu ikiwemo na Mpenzi wangu Maimuna kujifungua Salama lakini shida ilikuwepo kwa Yusira ambaye alikuwa ananitaka kimapenzi. "Usiwe na Wasiwasi mzee wangu nitajitaidi kufanya kila linalowezekana ili kuhakikisha nafanya kama wewe unavyotaka. Kama Mjukuu andika umepata na mimi nitaendelea kuwa Mwaminifu daima kwako"Nilimwambia mzee Hijirafu ili kumtoa wasiwasi Ingawa Kile ambacho nilikuwa naongea nacho hata mimi nilikuwa sina Uhakika kama nitaweza kukifanyikisha. Tulitumia kama Muda wa Nusu saa tofauti na mwanzo wakati tunaenda kwenye ule Ukimbi ndio tulifika nyumbani. Nakumbuka Mwanzo tulikuwa tumetumiwa Kama Muda wa saa moja hivi ila Muda ule tulikuwa tumetumia nusu saa tu. Tulipofika nyumbani tulishuka na Mzee wangu kisha tulianza kuingia Ndani. Tulipofika Ndani niliwakuta Yusira na Maimuna na wenyewe tayari wapo kwa mzee wangu ingawa sikujua walitumia Usafiri Gani. Hapo kwa mzee Tulikaa huku tukijadili mambo mengi sana ya kifamilia. Huwezi amini muda ule nilikuwa naonekana kama Mwanafamilia mkubwa sana pale na kila Wazo ambalo nilikuwa nalitoa lilikuwa linaungwa Mkono kwa asilimia kubwa sana. Hata Rafiki yangu Daudi ambae mtoto wa kiume wa mzee Hijirafu ambaye ilisemekana yeye ndio alimuonesha dada yake mimi ili nimuoe alikuwa ananiunga mkono mbaya. "Sasa shemeji unatakiwa kufungua biashara kubwa ambayo itakufanya watu wakujue. Unajua sasa hivi wewe ni mtu mkubwa sana kwenye Familia yetu hivyo lazima ufungue kitu kikubwa huko duniani watu wakutambue. Maana sasa hivi hata mimi nikihitaji pesa natakiwa nikuombe wewe. Utaamua Wenyewe maana Asilimia kubwa ya binadamu ambao hupewa mali na Majini wenyewe humilika sana Magari. Ila Ukiona binadamu anamahusiano na Majini alafu akamilika Magari Mengi sana Hususani mabasi unatakiwa uelewe kuwa huyu binadamu kaoa ukoo wa Majini ya Shauma ambayo kila baada ya Mwaka mmoja huhitaji damu za watu. Lakini bwana sisi Ukoo wetu ni Yauma hivyo hatutaki damu ya aina yeyote maana sisi ni waislamu na tunamuamudu Mungu kama wewe unavyomuabudu. Unajua CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Sisi majini hatuna utofauti sana na binadamu. Utofauti wetu ni kwamba sisi tunaishi chini ya bahari ambao ni kisiwani yani Ulimwengu wa Majini na Nyinyi Binadamu Mnaishi Duniani. Pia sisi Majini tunauwezo wa kuja Duniani Muda wowote tunaotaka bila kizuizi chochote lakini Nyinyi binadamua hamuwezi kuja kwenye ulimwengu wa majini HUSUSANI KISIWA CHA MAJINI kwa kujiamulia hadi uwe uletwe na Jini. Mimi naweza kusema hicho ndicho Mungu alichotupendelea. Ila kama Dini wote tukasawa Maana hata huku Kuna Majini Yenye imani ya Dini ya Kikristo na Majini yenye Iamani ya Dini ya Kislamu na yote yanaswali na yanajua Uhumimu wa kuwepo kwa Mungu. Pia kuna Majini ambayo haya dini Kabsa na yanamuhasi Mungu kama kuuawa Watu, kunywa Pombe na kufanya Anasa mbalimbali ambao hata Nyinyi kuna watu wanaofanya vitu kama hivyo. Mfano sisi kuna Aina flani ya Jini ambae tunamchukia sana kutokana na tabia yake ya kuwafanyia binadamu Unyama pamaja na Majini wenzake. Hawa Majini sisi Sisi tuna Muita TURUFAILA Ila nyinyi binadamua Mnapenda sana kumuita POPOBAWA. Huyu ni aina ya Jini ambae amelaniwa na Asilimia kubwa ya Majini ndio maana hata Mambo yake anafanya kishetani zaidi."Aliongea Daudi. Yale maneno ya daudi kwa kweli yalinifumbua akili kidogo na kubaini kumbe kuna mabasi Duniani Mengine wanaomiliki ni binadamu ambao wanamikakati ya Damu na Majini. Pia kumbe huyu popobawa ambae wanasema akikufanyia kitu usipomtangaze anakufanyia Tena kumbe alikuwa Jini ambaye amelaniwa na Majini wote. Pia kitu kingine ambacho kilikuwa Kina nisumbua kichwa ni Daudi kuniambia kuwa wao Ukoo wao ni Majini ya Yauma. Sasa kama wao ni Majini ya Yauma kwa nini waliniambia Mahali ya Kumuoa Ndugu yao Peninana natakiwa kumtoa kafala Mama yangu. Hapo kwa kweli nilianza kuamini huenda mama yangu Bado yupo ila kuna mchezo ambao nilikuwa nimechezewa. Sikutaka kuulizia Sana Hususani Swala la mama yangu maana nilikumbuka ni Moja ya kitu ambacho Maimuna alikuwa anakichukia sana. Maimuna alikuwa Hapendi kabsa kuona Mimi nakuwa napeleleze kuhusu mama yangu. Tuliongea Mambo Mengi sana na tulikubaliana kuwa Mimi nitaenda Kufungua Biashara ya Kuuza vifaa ya Magari, pikipiki, wakati Mwingine hata kuuza Magari pamoja na Pikipiki. Baada ya story za hapa na pale Ndefu sana Hatimae mimi na Mpenzi wangu Maimuna tulionyeshwa chumba ambacho tutapumzika siku mbili kabla ya kurejea Duniani. Muda wa saa mbili Usiku tayari tulikuwa tumeshakula na nilikuwa nipo kitandani na Mke wangu Maimuna tunashikana shikani. Wakati tukiwa tunashikana Mke wangu aliniambia kuwa Anahisi kichefuchefu na kuamka kwenda sehemu flani palepale chumbani ambapo kulikuwa na ndoo na kuanza kutapika. Wakati Maimuna akiwa anatapika kwa kweli nilishituka sana maana alikuwa anatapika Kwa mfululizo alafu matapishi yalikuwa damu tupu. Hata nilipoamka kitandani na kumsogelea nilikuta Ndoo ya lita kumi tayari ilikuwa imefika katikati alafu ilikuwa damu tupu. Ile hali kwa kweli ilinifanya kushituka na kuanza kutetemeka maana sikujua kwa nini ile hali imetokea vile. "Mume wangu wala usiogope, unajua baba yangu anahitaji mtoto ambae tutamzaa awe binadamu na siyo jini. Hivyo hapa ninavyotapika ndio mtoto anabadilika kutoka Ujini kuwa binadamu wa kawaida. Hivyo damu zote ambazo mtoto wangu anatumia pindi yupo tumboni kwangu na Dna za kijini zitamtoka na kubadilika kuwa binadamu wa kawaida."Aliongea Maimuna maneno yaliyonifanya kubaki nikiwa nimeduaa






 Kwa kweli yale Maneno ya Maimuna ndio kwanza yalizidi kunichanganya. Nilishindwa kuelewa ile damu kweli ambayo ilikuwa inatoka ilikuwa ya mtoto kutoka tumboni. Je kama kweli Ile damu ilikuwa inatoka ilikuwa mtoto Tumboni je yeye angebaki na Damu gani sasa. "Maimuna unajua unanichanganya sana damu yote hii unaniambia mtoto kutoka tumboni anabadilika kuwa binadamu wa kawaida. Hebu acha utani twende tufanye mpango wa kukupeleka hospitalini. Hata kama hii damu ya mtoto unataka kuniambia mtoto atabaki na nini sasa tumboni kama siyo kusababisha kifo chake"Nilimwambia Maimuna. "Hospitali ya nini Mume wangu hebu jaribu kunielewa kile ambacho mimi nakwambia. Hii damu inamtok a mtoto tangu mimba ilipoanza kutungwa hadi sasa hivi. Hivyo damu ambayo atakuwa anatumia mwanao sasa hivi inatakiwa kutoka kwako. Hivyo inatakiwa kila baada ya wiki moja tutakuwa tunakuja huku kisiwani wewe unatolewa Damu kisha mimi naongezewa ile damu ndio atakuwa anatumia mtoto wako ili kumfanya asije kuwa jini tena. Alafu wakati mimi najifungua mtoto unatakiwa uwe karibu sana maana siku najifungua mtoto atakuwa hana damu yeyote ile na wewe ndio ambae utatakiwa kumuongezea damu. Najua itakuwa vigumu sana kunielewa hichi ambacho nakwambia ila jifanye kama tayari umeshaelewa"Aliniambia Maimuna. Kupitia yale maelezo ya Maimuna kweli niliamua kujilazimsha na kujifanya kama nimeelewa ingawa bado sikumuelewa sana. Niliacha kama ilivyo maana nilikuwa Naamini kile ambacho anakiongea maimuna ni cha ukweli. Maana nakumbuka hata baba yake Mzee Hijirafu aliwahi kuniambia kuwa anapenda mtoto ambae tutapata awe binadamu na siyo jini. Maisha yaliendelea pale kisiwani hatimae tulimaliza siku zetu mbili na kurudi duniani. Tuliporudi Duniani tuliendelea na maisha ya kila siku. Zilipita siku kama tano hivi mambo yalikuwa safi na sikupata Usumbufu wowote kutoka kwa Yusira maana tulikuwa tumemuacha kisiwani. Muda ule tayari mimi tukishilikiana na shemeji yangu daudi tulikuwa tumefanya mawasiliano ya kutafutiwa nyumba kubwa dar kwa ajili ya kufanyia biashara zangu. Ukimya wa Yusira ulinifanya kubaini kama kile kitu ambacho alikuwa amepanga kukifanya alikuwa ameacha. Nakumbuka ilikuwa siku ya juma Pili ambae zilikuwa zimekatika wiki kama tatu hivi tangu tutoke kisiwani. Hiyo siku Maimuna aliamka mapema sana na kwenda kwenye biashara zake na kuniacha peke yangu. Siku hiyo mimi nilikuwa nimejichokea sikutaka kumfuata maimuna maana nilijua Muda wa saa sita tu tayari atakuwa amesharudi maana ile siku ilikuwa juma pili na huwa anafunga ofisi mapema sana. Hata wakati anaondoka Maimuna aliniambia anawahi kurudi na anahamu sana kuja kucheza na mimi na kufanya mapenzi kwani siku zake za kustopisha kufanya mapenzi zilikuwa zimekaribia maana mimba nayo ilikuwa inatakribani miezi mitano. Muda wa saa sita hivi tayari Maimuna alisharudi na tulikuwa tupo kitandani wote tumevuana Nguo na ilibaki kumlaza vizuri Maimuna ili kumpiga mapigo ya kimimba mimba. "Huu ndio Muda wangu wa kunipatia kile ambacho nahitaji maana muda wangu wa kurudi saudi umeshafika" yalikuwa ni maneno ambayo yalinishitua sana. Kumbe yule mtu ambaye tulifikia hadi kuvua nguo alikuwa ni Yusira na wala siyo Peninna




CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kwa kweli nilipobaini yule mtu ambae nilikuwa nataka kufanya nae mapenzi hakuwa Maimuna bali ni Yusira nilishituka sana. Mapigo yangu ya moyo yalibadilika ghafla na woga wa ajabu ulianza kuniingia. Nilikumbuka maneno ya Maimuna ambayo aliwahi kuniambia kama nitafanya mapenzi na mwanamke wa aina yeyote yule nitageuka mbwa ndio nilizidi kuchanganyikiwa zaidi. Kama hiyo haitoshi nilikumbuka pia maneno ya baba yake na Peninna mzee Hijirafu aliyoniambia kuwa Muda huu natakiwa niwe makini nisifanye mapenzi na mwanamke wa aina yeyote yule. Kama ikitokea nikafanya basi nitakosa utajiri wa kijini kwani tayari nitakuwa Mchafu pamoja na kumuua Mwanangu ambaye alikuwa tumboni. Nilipo kumbuka yale maneno yote nilikurupuka kitandani na kushuka huku nikitaka kutoka chumbani nduki vile vile nikiwa uchi. Kwa kweli Swala la kufanya Mapenzi na Yusira kwangu nilikuwa naona hatari sana na kitu ambacho hakiwezekani milele. Maana kufanya mapenzi na yusira ulikuwa kama ndio mwisho wa Maisha yangu. Nilipokurupuka pale kitandani nilianza kuufuata Mlango wa kutokea chumbani kwangu kwa kasi ya ajabu ili nitoke hata nje. Cha ajabu wakati nakaribia kuufikia mlango nilishangaa mkono wa mtu unanipita na kwenda kushirikilia ule mlango. Ilibidi nigeuke nyumba kuangalia Yusira kashaamka nini na yeye ili kuja kuzuia mimi kutoka. Nilipoaangalia Nyuma cha ajabu yusira alikuwa amekaa tu kitandani huku mkono wake ndio aliunyosha kwenda kuzuia ule mlango. Yani mkono wake uliongezeka urefu kiajabu ajabu ambae hata mimi sikuwaza kama kuna mtu duniani ambae anauwezo wa kuwa na mkono mrefu kama ule. "Nahitaji kutoka Yusira, nahitaji kutoka nje yusira siwezi kufanya kile ambacho unakitaka tafadhari. Yusira kumbuka kuwa kufanya mapenzi na wewe unazidi kuniweka kwenye wakati Mgumu sana, Nikifanya Mapenzi na wewe Yusira kwanza Mwanangu tumboni kwa Maimuna atakufa, pili nitageuka kuwa Mbwa na tatu ukoo wenu wa Majini hautanitaka tena. Tafadhari bado nahitaji kuwa binadamu, bado nahitaji kuwa na Maimuna, bado nahitaji kuwa miongoni mwa member ya familia yenu na nahitaji kuwa na mtoto Yusira tafadhari nakuomba niache"Nilimwambia yusira kwa sauti ya huruma huku muda ule hadi machozi yalianza kunitoka. Cha ajabu pamoja na kuongea hadi Machozi kuanza kunitoka lakini Yusira yeye alianza kucheka tena kicheko ambacho kilikuwa kikali sana. Nilishindwa kuelewa Yusira alikuwa mtu wa Namna gani namwambia maneno ambayo yalikuwa yaukweli na yalikuwa yananiumiza mimi yeye anacheka. "Pole sana kapopo kwa kuwa na mawazo ya kijinga namna hiyo. Naomba unisikilize kwa Makini Kapopo. Hivi wewe ukoo wetu wa majini unakuhusu nini, wewe ni binadamu na unaukoo wako kabsa sasa unataka na ukoo wa majini ili iweje sasa. Kule ulioa Kapopo tena dada yangu ulimchukua bure kabsa hata hujamlipia kitu chochote. Kuhusu kufanya mapenzi na Mimi ukabadilika at kuwa Mbwa huo sio ukweli maimuna alikuchimba biti tu. Maimuna anakupenda sana hawezi kukuwekea Mtego kama huo. Hata kama kweli kaweka mtego huo unatakiwa Utambue kuwa huo mtego hadi ufanye mapenzi na binadamu mwenzio ndio unakuwa mbwa ila siyo jini. Kuhusu hilo kwa kweli usiwe na tabu kabsa ninauhakika hautabadilika kuwa mbwa hata kidogo kuwa huru maimuna alikuwa anakudanganya tu. Kuhusu mtoto wako kufa tumboni hilo kweli linaweza kufanyika ila sasa mimi sina jinsi. Hata kama Mwanao atakufa tumboni utazaa mwingine tena mzuri tu na binadamu mwenzako ambae hata kuwa na hatua za kubadilika kutoka ujini kuwa binadamu wa kawaida. Kuhusu kutengwa na Ukoo wa kijini kwa kweli mimi hilo halinihusu sana maana najua wewe ni binadamu hivyo Masuala ya kuniambia unaogopa kutengwa na ukoo wetu hilo nakushangaa. Ulimzoe mzee hijirafu siyo na umepapenda sana kisiwa cha majini, huko siyo kwenu kapopo kwenu ni huku duniani"Aliongea Yusira Maneno ambayo yalinifanya hadi nilianza kutetemeka. Nilishindwa kuelewa Yusira alikuwa Jini gani ambae alikuwa na roho mbaya namna ile alikuwa yupo tayari kuona Mtoto wa dada yake Maimuna ambae bado alikuwa yuko tumboni anakufa kisa ati tufanye mapenzi na yeye. Nilishindwa kabsa kumuelewa maana nilihisi maisha yangu yanaelekea kubaya. Pia kitendo cha kuniambia kuwa mimi nimemuoa Maimuna bure kilizidi kunitatiza kidogo maana nilimua mama yangu ili kuweza kumuoa maimuna. Kumbukumbu ya Maneno matamu ya Mzee Hijirafu yalinielejea kichwani mwangu kipindi ananikabidhi utajiri na kunitambulisha kama mwanae ndio nilizidi kuchanganyikiwa ziadi. "Yusira tafadhar nakuomb niache nahitaji sana kuendelea kuishi na Maimuna. Tafadhari nahitaji kumpatia Mzee wako Mjukuu kama yeye ambae aliniambia. Nipo tayari kukutafutia mtu mwingine ufanye nae mapenzi maana ninarafiki wengi kama Mdete ,Maulid ilimladi mimi uniache"Nilimwambia tena Yusira ambae sasa mkono wake ulikuwa umesha achia mlango na alikuwa amenishika mkono wangu. "Binadamu wengi sana na wazuri wananihitaji ila mimi nimekuchagua wewe. Nahitaji kufanya mapenzi na wewe na wala siyo binadamu mwingine"Alinijibu Yusira na kunivuta kwa Nguvu na kunirudisha hadi kitandani. Yusira aliponivuta kwa Nguvu kunirudisha kitandani alinikaba mbaya kwenye koo. Kitendo cha kunikaba kwenye koo nilishangaa kuanza kuona hisia kali sana ya mapenzi ikinijia huku hamu ya kutaka kufanya mapenzi na Yusira ilianza kuja kichwani mwangu. Nilijikuta naanza kujilaumu kwa nini nilikuwa namsumbua Yusira. Yani ile Nguvu ilikuwa ya ajabu sana maana kila kitu kuhusu mtoto wangu kufa, kugeuka mbwa vilifutika akilini kwangu."Yusira baby nimekuumiza, nahitaji kukupa penzi tamu mamy"Nilijikuta naongea maneno ambayo sikujua ilikuwaje hadi kufikia kuongea vile. Yusira aliendelea kunishika kwenye koo kama muda wa dakika moja na kuniachia. Aliponiachia Moja kwa Moja nilifikia kuanza kupapasana maana nilikuwa na mzuka wa Ngono mbaya na Mashine yangu ilikuwa imesimama vilivyo. Tayari Yusira alishaniteka kinguvu za majini na nilikuwa sina Jinsi tena maana hakuna ambacho nilikuwa nakumbuka kama kufanya mapenzi na Yusira ilikuwa ni hatari. Tuliendelea kupapasana pale huku mdomoni tukiwa tunabadilishana mate hatimae nilimuweka Yusira vizuri na kuchomeka mashine yangu ndani ya Tunda la Yusira. Kitendo cha kuchomeka Mashine nilishangaa kuona kama Taswira ya maimuna inanijia karibu yangu huku akilia na kulalamika kapopo umemuua mwanao. Nilijitaidi kuitafakari ile taswira lakini ilikuwa haiji na utamu wa yusira ulinizidi zaidi.




Kwa kweli Penzi ambalo nilikuwa napatiwa na Yusira lilikuwa la aina yake ambalo lilinifanya kusahau kabsa kama lile Penzi ambalo nilikuwa nalifanya lilikuwa la hatari sana. Nguvu za kijini za Yusira zilikuwa zimenilemea Sana na nilikuwa sina Jinsi. Yusira alikuwa ni Fundi wa Mapenzi mbaya maana Hata wakati tunafanya Mapenzi yeye alikuwa hakai mikao ya kawaida. Ilikuwa mimi nalala chini kisha yeye anakalia Mashine na kuanza kuchezesha kiuno. Yani pale mimi ndio nilikuwa nafundishwa style zamapenzi. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/Usumbufu ulikuwa kibao maana ukifanya hii mara unaamshwa na kuambiwa kaa kwenye stuli kisha anakuja kukukalia. Yani kweli ule nilikuwa napata Utamu ambae ulikuwa umepitiliza hadi unazalisha uchungu. Maana baada ya kumaliza kufanya mapenzi na Yusira kuna kitu kibaya kilikuwa kinatakiwa kutokea. Tayari mimi nilishaenda kimoja ila sikujua Yusira yeye alikuwa ameenda vingapi maana yeye ndio alikuwa amenogewa zaidi na kujibalance utafikilia tulikuwa tunafanya mapenzi chumbani kwake. Muda ule mimi nilikuwa sina jinsi maana nilikuwa naongozwa kama roboti. Nakumba tulikuwa tumelala style ya Mwisho ambae ilikuwa kali sana. Ile style inaitwa KAMUA YOTE maana mkilala pale inamaana mnataka kufanya mapenzi na kujifunga koli haraka. Ile style Yusira alilala kifudifudi kisha kwenye kitovu aliweka mto ambae ulimfanya sehemu zake za siri kunyanyuka kidogo. Mimi nilikuja kumlalia juu kidogo na kufanya kama namtanua miguu yake huku nikiwa naikunja alafu nikachomeka mashine yangu. Ila style huwa ni Funga kazi na humalizi dakika tatu bila kujifunga goli. Niliendelea kumpiga yusira kwa kasi ya ajabu maana utamu ulishakaribia kutoka. Ile sasa nasikia kitu kinatema cheche huku na Yusira akipiga kelele za kusema na yeye anamwaga nilisikia kama Mlango wa chumbani kwetu ukifunguliwa na vishindo vya mtu vilisikika akitembea kwa kasi kuja kitandani. Kwa ule utamu kwa kweli sikuweza hata kugeuka kuangalia alikuwa nani zaidi ya kukaza mashine yangu ndani ya tunda la Yusira ili cheche zitemwe vilivyo. "Kapopo umemua Mwanangu, nasema umemua Mwanangu tumboni"zilikuwa ni kelele za Maimuna zikiambatana na vibao vya Mgongoni ambavyo vilinishitua mimi pamoja na Yusira. Niliposikia zile kelele kichwani kwangu kama kitu kilitoka hivi ghafla kumbukumbu zilinirudia na kukumbuka kila kitu. Kwa kweli nilishindwa nifanye nini na kubaki nikiwa nimedua kitandani huku machozi naye yakianza kunitoka. "Yusira niambie tumefanya nini na wewe, tafadhari niambie kuna kitu tumefanya na wewe"Nilimwambia yusira huku nikiwa nimemkaba mbaya na mwili wote ulikuwa unatetemeka. Yusira nae alikuwa amechanganyikiwa mbaya maana hata kuvaa nguo aliona tabu alibaki amekodoa macho na kushikashika nywele zake. "Kapopo nimekukosea nini mimi hadi unaniadhibu namna hii, kapopo kumbuka mwanangu tumboni atakufa na hautakuwa wangu tena umevunja mashariti ya kijini. Kitu gani ambacho ulikikosa kapopo kwangu"Aliongea Maimuna huku akiwa analia mbaya. Kwa kweli ile hali ilinifanya hadi mimi kuanza kulia maana mimi ndio nilikuwa kwenye hatari zaidi. "Maimuna naomba nisamehe sana sina jinsi kwa kweli sijui nikwambie nini ili unielewe. Maimuna mimi sikuwa tayari kufanya mapenzi na Yusira ila amenilazimisha kwa kutumia Nguvu za kijini ambazo zilinifanya nisahau na kujikuta nafanya mapenzi. Maimuna hii siyo mara yetu ya kwanza hata kule Saudi Arabia tulifanya mapenzi na yusira kwa kunilazimisha hivi hivi kutumia Nguvu za kijini. Unakumbuka hata kipindi nilipotaka kutoroka nyumbani kipindi yusira anakuja nilitaka kumkwepa Maana alikuwa anakuja kwa nia ya kufanya mapenzi. Sijakusaliti maimuna ila Yusira ndio amenifanya nikusaliti na nimefanya mapenzi bila akili yangu"Nilimwambia Maimuna huku nikiwa navaa nguo zangu. Ambacho kilinishangaza yale maneno ambayo nilikuwa namwambia Maimuna aliyaelewa tofauti na Mwanzo kila nilipokuwa namueleza alikuwa hanielewi. Kwa kweli nilishindwa kuelewa kwa nini leo Maimuna kanisikia hiki ambacho nakiongea siku zote namwambiaga hanisikii. "Mdogo wangu kweli umeamua kunifanyia hivi, mdogo wangu umeamua kumuua hadi mtoto wangu tumboni kisa mapenzi. Mbona wanaume wako wengi yusira, ungeacha basi nijifungue salama ndio ungeniadhibu hivi"Aliongea Maimuna huku akiwa analia na kutoka chumbani kwa kasi mbaya. Muda ule Yusira alikuwa kama kachanganyikiwa hivi maana alibaki kitandani akiwa ametulia kimya huku hata kuvaa nguo alikuwa hataki. Baada ya muda kama wa dakika mbili hivi kupita Maimuna alirudi chumbani huku akiwa na kisu cha ajabu sana. Kile kisu nilipokiangalia kilikuwa chekundu kama kilikuwa kimewekwa kwenye moto wa mkaa mkali sana. "Yusira lazima nikuue huwezi kumuua mwanangu na kunifanya nimkose kapopo. Kumbe umemlazimisha Mume wangu kwa kutumia nguvu za kijini. Najua unanguvu sana kunishinda mimi ila hii kisu ndio kiboko yako. Nitakuua wewe kisha mimi nae nitajiua na kumuacha kapopo huru kwani hana hatia. Hukupaswa kuniazibu hivi Yusira hukupaswa kabsa Kunifanyia Unyama kama huu"Aliongea Maimuna Maneno yalinimfanya Yusira kushituka na kumwangalia. Wakati nikiwa nashangaa ile hali na kutaka kumzuia Maimuna asifanye hivyo tayari alishaamfata Yusira kwa kasi ya ajabu ili kwenda kumkita kile kisu. Kwa kweli hadi sasa bado huwa najiuliza sijui nguvu gani Yusira ambazo alitumia maana Ndani ya sekunde tano kabla Maimuna hajamfikia sijui alijigeuzaje na kubadilika ghafla akawa na mavazi meupe yote kuanzia juu hadi chini. Kitendo cha maimuna kunyoosha kisu ili kumchoma nilishangaa Yusira anakishika kile kisu kwa Maajabu na kumchomo Maimuna tumboni. Wakati nashangaa ile hali Yusira alipotea pale Ghafla.


INAENDELEA

No comments

Powered by Blogger.